Samia ashiriki uzinduzi Global Africa Investment Summit

RAIS Samia Suluhu Hassan ameshiriki uzinduzi wa Global Africa Investment Summit (GAIS) jijini Dubai, Muungano wa Falme za Kiarabu (UAE), mkutano ulioashiria hatua mpya ya Afrika katika kuvutia mitaji ya kimataifa kupitia uwekezaji uliopangiliwa na wenye uhalisia wa kifedha.

Kwa mujibu wa Ikulu, akihutubia mkutano huo, Rais amesisitiza kuwa wawekezaji hawatafuti fursa pekee, bali uaminifu – uthabiti wa sera, taasisi imara na serikali zinazotekeleza ahadi zake.

Ameeleza namna Tanzania imewekeza kimkakati katika nishati, reli, bandari na miundombinu ya uchukuzi, pamoja na Maeneo Maalum ya Uwekezaji na Dirisha Moja la Uwekezaji, ili kujenga mazingira rafiki kwa wawekezaji wa muda mrefu.

Ushiriki wa Tanzania katika GAIS unaakisi dhamira ya nchi ya kwenda kwenye ushirikiano uliopangiliwa vizuri na unaoendana na vipaumbele vya maendeleo ya taifa na matarajio ya wawekezaji wa kimataifa.

GAIS inalenga kuoanisha uongozi wa kisiasa, rasilimali za kitaifa na mitaji ya kimataifa, na kuifanya Afrika – na hususan Tanzania – kuwa kitovu cha uwekezaji unaoleta matokeo, ajira na maendeleo endelevu.

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button