Serikali mbioni kusaini mkataba wa LNG

Sh trilioni 70 kuleta mapinduzi ya kiuchumi

SERIKALI ipo hatua za mwisho za maandalizi ya kusaini mkataba wa  mradi wa Kuchakata na Kusindika Gesi Asilia (LNG) na wawekezaji Kampuni ya Shell ya Uholanzi na Equinor ya Norway .

Hayo yamesemwa leo Julai 3, 2023 Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati Mhandisi Felchesmi Mramba katika mdahalo ulioandaliwa na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade), kuhusu mafuta na gesi asilia uliofanyika katika Maonyesho ya 47 ya  Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba).

Amesema, uwekezaji wa mradi huo ni  zaidi ya Shilingi Trilioni 70 utaleta mapinduzi makubwa ya kiuchumi nchini na utaifanya Tanzania kuwa moja ya nchi zinazochangia katika usalama wa nishati dunia.

Mramba amesema, mradi huo wa kuchimba Gesi Asilia katika eneo la Bahari Kuu Kusini mwa Tanzania katika eneo la Likong’o Lindi utakuwa na faida kubwa kwa nchi, ni mradi ambao serikali inatarajia utabadilisha pato la taifa (GDP).

“Uchumi wa nchi yetu na maisha ya watu yatabadilika. Utazalisha ajira, utatoa fursa ya kuweka viwanda vingine, ni mradi ambao utaongeza kiasi cha gesi ambacho kitatumika ndani ya nchi, na kitakachouzwa nje na kuingiza fedha nyingi za kigeni.” Amesema Mramba

Amesema, gesi asilia ambayo Tanzania imegundua kiasi kikubwa kipo baharini, gharama ya kuitoa Baharini ni kubwa umbali wa kutoka nchi  kavu kuingia ndani ya Bahari mpaka kufika maeneo ya vile visima, ni kati ya kilometa 120 mpaka 250  ni ndani sana na unaikuta gesi ikiwa kwenye kina kirefu cha Bahari.

“Gharama za uwekezaji ni kubwa  lakini huu ndio muda muafaka wa kuvuna rasilimali hiyo ambayo Mungu ameibariki nchi yetu.”Amesema na kuongeza

“Msisahau gesi asilia duniani inatajwa kama nishati mbadala, tunapoelekea dunia inaenda kuhama kutoka kwenye gesi ya hewa  ukaa na kutumia nishati ambazo hazizalishi hewa ya ukaa. matumizi ya mafuta na gesi tunapokwenda yataenda kupungua.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
3 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Juliat
Juliat
2 months ago

Make everyone ( $26,000 __ $38,000 ) A Month Online Making money c7 online more than $20k just by doing simple work With No Prior Experience Or Skills Required. Be Your Own Boss And for more info visit any tab this site Thanks a lot just
open this link.======> http://getjobz12.blogspot.com

Last edited 2 months ago by Juliat
Julia
Julia
2 months ago

Earn income while simply working online. work from home whenever you want. just for maximum 5 hours a day you can make more than $600 per day online. From this i made $18,000 last month in my spare time.
.
.
Detail Here—————————————————————>>>  http://Www.OnlineCash1.Com

Lori L. Kent
Lori L. Kent
2 months ago

I am making easily every month $ 22000 to $ 28000 just by doing simple work from home. This job is online and very easy to do part-time or Full-time even no special experience required for this task. h96 Anyone can now participate in this job and start earning just like me by just click this link….. http://www.pay.hiring9.com

Back to top button
3
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x