DODOMA – Tanzania imesema askari wake wawili wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi (JWTZ) waliokuwa wakishiriki shughuli za ulinzi wa amani wameuawa kufuatia shambulio la Waasi wa M23 huko Goma, nchini DRC.
JWTZ imesema kupitia taarifa kwa vyombo vya habari kuwa katika shambulio hilo wanajeshi wengine wanne wamejeruhiwa.
“Taratibu za kuisafirisha miili ya marehemu pamoja na majeruhi zinaendelea kupitia Sekretarieti ya SADC,” Kanali Gaudentius Ilonda, Kaimu Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania amesema.
Ameeleza kuwa wanajeshi hao walikuwa sehemu ya kikosi cha ulinzi wa ama cha Umoja wa Mataifa na Jumuiya za Kikanda.
Kwa mujibu wa Kanali Ilonda, vikundi vya Tanzania vilivyopo DRC vipo salama, imara na vinaendelea kutekeleza majukumu yake kwa maelekezo ya uongozi wa SADC .
JWTZ limeshiriki kulinda amani katika nchi mbalimbali ikiwemo Lebabon, Sudan, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Liberia, Msumbiji, na DRC.
Rest In Peace Wapambanaji
Hi there! Do you use Twitter? I’d like to follow you
if that would be ok. I’m undoubtedly enjoying your blog and look forward to new posts. https://xeuser.gajaga.work/index.php?mid=board&document_srl=173264