Simba yafunguka kocha mpya

KLABU ya Simba imesema itatumia kipindi cha mapumziko kupisha ratiba ya michuano ya fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON) zinazotarajiwa kuanza Morocco Desemba 21, mwaka huu kutafuta kocha wa kuinoa timu hiyo.
Simba ambayo iliachana na Meneja wake Mkuu, Dimitar Pantev iko chini ya kocha Selemani Matola akikamilisha ratiba ya mechi za Ligi Kuu leo kwa kuikabili Azam, Uwanja wa Benjamin Mkapa kabla ya kwenda mapumziko.
Akizungumza na HabariLEO hivi karibuni, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally alisema watatumia kipindi cha mapumziko kupisha michuano ya Afcon kutafuta kocha atakayekuja kukinoa kikosi chao.
Alisema kwa sasa timu hiyo itakuwa chini ya kocha Selemani Matola kwa muda mpaka pale mchakato wa kumpata kocha mpya utakapokamilika kipindi hiki cha mapumziko kupisha michuano ya Afcon.
“Matola atamalizia mechi yetu ya leo dhidi ya Azam na baada ya hapo tutatumia kipindi hiki cha mapumziko kusaka kocha mpya,” alisema Ahmed.
Aidha, Ahmed alielezea dhamira yao ya kufanya vizuri kwenye michuano ya ndani na ya kimataifa msimu huu licha ya kuanza vibaya kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika.
“Tumeanza vibaya michuano ya Ligi ya Mabingwa lakini hii sio mara ya kwanza kwetu, tuliwahi kuwa kwenye hali kama hii lakini msimu huu tumepania kufanya vizuri kwenye mashindano ya ndani na ya kimataifa,” alisema Ahmed.
Simba imepoteza mechi zake mbili za Ligi ya Mabingwa Afrika kwa kufungwa bao 1-0 na Petro de Luanda, Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam kabla ya kukubali kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa Stade Malien, Bamako, Mali.




Single Mom Reveals How She Earns $89k/Yr Working 10 Hrs/Week From Home. Tired of paycheck-to-paycheck living? Meet Kelly from New York—a regular mom who cracked the code to recession-proof income without selling a thing! Now,Big thanks …
.
Here is I started____________________ http://Www.Cash43.Com
Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
.
More Details For Us→→→→→→→→→→ https://Www.Payathome9.Com