Singida BS yapenya makundi CAF

DAR ES SALAAM; TIMU ya soka ya Singida Black Stars ya Tanzania imetinga hatua ya makundi Kombe la Shirikisho Afrika baada ya kuifunga Flambeau Du Centre ya Burundi mabao 3-1 katika mchezo yliofanyika leo Uwanja wa Azam Chamazi, Dar es Salaam.
Mchezo wa kwanza baina ya timu hizo uliofanyika nchini Burundi, timu hizo zilitoka sare ya bao 1-1, hivyo Singida BS kusonga mbele kwa jumla ya mabao 4-2.



