Taasisi yakabidhi watoto vifaa vya shule

DAR ES SALAAM; Taasisi ya kidini ya Al Ameen Foundation (AIF) ya Kijitonyama, Dar es Salaam, imekabidhi vifaa vya shule kwa watoto Kijiji cha Magoza, Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani.

Mwenyekiti wa taasisi hiyo, Ghalib Monero amesema shughuli ya ugawaji vifaa hivyo ilifanyika kwenye kijijini hapo Januari 3, 2026 na kuhudhuriwa pia na baadhi ya viongozi wa madrasa na msikiti Sabera.

“Nikiambatana na baadhi ya wanachama wa Taasisi ya Al Ameen Foundation tumegawa madaftari kwa watoto wetu wa Madrasatul Sabera iliyopo Kijiji cha Magoza, Mkuranga, Pwani,” amesema na kuwataja baadhi ya wazee wa madrasa na msikiti Sabera waliohudhuria tukio hilo kuwa ni Sheikh Kassim Kyuta na Mohamed Mpetuka.

Amsema kukabidhi vifaa hivyo kunafuatia mkakati ulioanzishwa na taasisi yake kwa kuhusisha wadau mbalimbali katika programu maalumu iitwayo Vifaa Shule 2026, ambapo wanachama wa taasisi hiyo huchangia ili kusaidia watoto wakiwemo yatima.

“Tukio kubwa zaidi litafanyika Januari 10, 2026 ofisini kwetu Al Ameen Foundation Kijitonyama, ambapo pia tutatoa vifaa mbalimbali ikiwemo madfatari na kalamu kwa watoto,” amesema Monero na kuongeza kuwa taasisi yake ni ya kidini inayohusika na masuala mbalimbali ya kijamii.

Habari Zifananazo

2 Comments

  1. l Get paid over $110 per hour working from home. l never thought I’d be able to do it but my buddy makes over $21269 a month doing this and she convinced me to try. The possibility with this is endless….

    This is what I do………………………………….. https://Www.Cash54.Com

  2. Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
    .
    M­­­­­­o­­­­­­r­­­­­­e­ D­­­­­­e­­­­­­t­­­­­­a­­­­­­i­­­­­­l­­­­­­s For Us→→→→→→→→→→ https://Www.Payathome9.Com

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button