Taasisi za serikali 369 zasitisha matumizi ya mkaa, kuni

TAASISI za serikali zipatazo 369 zimeunga mkono agizo la Ofisi ya Makamu wa Rais ,Muungano na Mazingira kwa kuacha kutumia nishati ya kuni na mkaa na badala yake kuingia katika matumizi ya nishati safi na salama ya gesi.

Meneja wa mauzo kwa wateja  wa Kampuni  ya Taifa Gas Tanzania Limited , Moses Massawe amesema  hayo  Juni 15, 2023  wakati wautoaji  mafunzo  kwa waandishi wa habari wa Mkoa wa Morogoro kuhusu kampeni ya utunzaji wa mazingira na matumizi ya nishati safi  na salama ,tukomeshe uvunaji wa miti kiholela.

Massawe amesema kampuni hiyo inaunga mkono juhudi za serikali katika suala la uhifadhi na utuzaji wa mazingira hivyo imeweka mkakati wa utoaji wa elimu juu ya madhara ya matumizi ya kuni na mkaa.

Advertisement

Amesema  kutokana na  elimu inayotolewa na kuendelea kutoleaa tayari  taasisi  369 za umma  imeunganishwa na matumizi ya  nishati safi na salama ya gesi.

“ Hadi sasa tumezifikia taasisi 369 za umma  ambazo zinatumia nishati safi  na salama  na katika mkoa wa Morogoro zipo taasisi nane zimeunganishwa na matumizi haya  na hivyo zimeondokana na kutumia  kuni na mkaa.” amesema  Massawe

Massawe amesema katika kukabiliana na changamoto hizo, Taifa Gas  kuanzia Julai hadi Disemba mwaka huu imeweka  mkakati  kuzifikia taasisi 460  na hivyo kufanya jumla ya taasisi 829.

Naye Mkuu wa Chuo cha Ualimu Morogoro , Augustine Sahili ambaye chuo chake limeachana na matumizi ya kuni na mkaa baada ya kuunganishiwa nishati safi na salama (Gas) alisema tabngu kuanza kutumia nishati hiyo wameweza kuokoa milioni 15 kwa mwaka .

“Tunapika chakula kwa muda mfupi  na nafuu kuliko mkaa na kuni  ambapo kwa mwezi ni Sh milioni 4.5  hadi sh milioni 4.8 na sasa tunatumia Sh milioni tatu  kwa matumizi ya gesi  na hivyo kuokoa sh milioni 15 kwa mwaka” amesema  Sahili

Mei 18, 2018 Serikali kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais iliangiza taasisi za serikali na mashirika yasiyo ya kiserikali  na mengine yenye matumizi makubwa ya kuni na mkaa, yatumie nishati mbadala kwa kupikia ikiwa ni njia mojawapo ya kupunguza uharibifu wa mazingira.

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *