MKUTANO wa 51 wa Baraza la Haki za Binadamu unaendelea Geneva, Uswisi, huku ujumbe kutoka Tanzania unaongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Prof. Eliamani Sedoyeka.
Mkutano huo ulianza jana Jumatatu na unatarajiwa kumalizika Oktoba 7, mwaka huu.
Taarifa iliyotumwa kwenye vyombo vya habari, inasema kuwa miongoni mwa ajenda ambazo Tanzania imejipanga kuzungumzia ni pamoja na haki ya maendeleo kwenye elimu, afya, makazi, maji salama na usafi.
Pia mkutano huo utazungumzia athari za Uviko 19, hasa katika sekta na mikakati madhubuti iliyowekwa ya kudhibiti uchumi dhidi ya janga hilo, ikiwemo kuhimiza utoaji wa chanjo ya uviko na kutangaza nchi kupitia Royal Tour.