Trump akana kubatilisha matokeo uchaguzi 2020

RAIS wa 45 wa Marekani, Donald Trump amekana mashtaka ya kubatilisha matokeo ya uchaguzi wa 2020 nchini Marekani.
Trump alitokea kwa mara ya kwanza jana mahakamani hapo ambapo alisema: “Unapoangalia kile kinachotokea, haya ni mateso ya mpinzani wa kisiasa, hii haikupaswa kutokea Amerikaโ.
Trump aliomba kesi hiyo inayoskilizwa katika Mahakama ya Barrett Prettyman ya huko Washington, DC kusikilizwa siku nyingine na hakimu alikubali kesi hiyo kusikilizwa tena Agosti 28.
Trump anashtakiwa ikiwa ni siku mbili tu baada ya waendesha mashtaka wa Marekani kuwasilisha mashtaka manne dhidi ya Trump, wakimtuhumu mwanasiasa huyo wa chama cha Republican kutaka kutengua matokeo ya uchaguzi wa 2020 ambao alishindwa na mpinzani wake wa chama cha Democratic, Joe Biden.
Kesi hiyo ni ya tatu kufunguliwa mashtaka ya jinai dhidi ya rais huyo wa zamani tangu Machi.
Trump pia anakabiliwa na mashtaka ya serikali huko New York juu ya madai ya malipo ya kimya kimya kwa nyota wa filamu na mashtaka ya serikali yanayohusiana na tuhuma kwamba alishughulikia vibaya hati za serikali huko Florida.
Trump amekanusha makosa yote na kudai kuwa mashtaka hayo ni majaribio ya kuvuruga kampeni yake.
๐๐๐ค๐ $๐,๐๐๐-$๐๐,๐๐๐ ๐ ๐๐จ๐ง๐ญ๐ก ๐๐ง๐ฅ๐ข๐ง๐ ๐๐ข๐ญ๐ก ๐๐จ ๐๐ซ๐ข๐จ๐ซ ๐๐ฑ๐ฉ๐๐ซ๐ข๐๐ง๐๐ ๐๐ซ ๐๐ค๐ข๐ฅ๐ฅ๐ฌ ๐๐๐ช๐ฎ๐ข๐ซ๐๐. ๐๐ ๐๐จ๐ฎ๐ซ ๐๐ฐ๐ง ๐๐จ๐ฌ๐ฌ ๐๐ง๐ ๐๐ก๐จ๐จ๐ฌ๐ ๐๐จ๐ฎ๐ซ ๐๐ฐ๐ง ๐๐จ๐ซ๐ค ๐๐จ๐ฎ๐ซ๐ฌ .
.
.
.
๐๐ข๐ฆ๐ฉ๐ฅ๐ฒ ๐๐๐ ๐ข๐ฌ๐ญ๐๐ซ๐ ๐จ๐ง ๐ ๐ข๐ฏ๐๐ง ๐๐๐โฆโฆโฆโฆ. http://www.join.salary49.com