UJERUMANI : ALIYEWAHI KUWA Rais wa Ujerumani Horst Köhler amefariki dunia leo jumamosi (01.02.2025) baada ya kuugua kwa muda mfupi.
Köhler aliyeiongoza Ujerumani kati ya mwaka 2004 hadi 2010, alifahamika kama muungaji mkono mkubwa wa bara la Afrika na amefariki akiwa na umri wa miaka 81.
Rais wa sasa wa Ujerumani Frank Walter Steinmeier amesema taifa lake limempoteza mtu muhimu aliyefanya mambo makubwa kwa nchi na dunia yote.
Kansela Olaf Scholz ametuma pia salamu za rambirambi kufuatia msiba huo na amemwelezea Rais huyo wa zamani wa Ujerumani kama “mwanasiasa mwenye kujitolea aliyefanya kazi kwa ajili ya kuimarisha haki duniani.
Kabla ya kuwa Rais wa Ujerumani, Horst Köhler alikuwa Mkuu wa Shirika la Fedha duniani IMF pia alishika wadhifa wa Urais baada ya kupendekezwa na kiongozi wa upinzani wa wakati huo Angela Merkel ambaye baadaye alikuwa Kansela.
SOMA: Ujerumani yaitisha uchaguzi mpya
If you desire to get a good deal from this post then you have to apply
such techniques to your won web site.
Hi there, of course this post is in fact fastidious
and I have learned lot of things from it concerning blogging.
thanks.
my webpage – Buy Bitcoin online