Urusi Ukraine wabadilishana mamia ya wafungwa

URUSI : MAMIA ya wafungwa wa Urusi na Ukraine wameachiliwa  huru  kupitia mpango wa kubadilishana wafungwa  uliosimamiwa na Umoja wa Falme za Kiarabu.

Rais wa Ukraine Volodymir Zelensky amethibitisha hilo na kusema kuwa wafungwa 189 wa Ukraine, wakiwemo maafisa wa kijeshi, walinzi wa mpaka na walinzi wa kitaifa pamoja na raia wawili, wameachiwa.

Huku Wizara ya Ulinzi ya Urusi nayo ikithibitisha na kusema kuwa askari 150 wa Urusi wameachiliwa huru kama sehemu ya ubadilishanaji huo ambao kila upande uliwaachia watu 150.

Advertisement

Hatahivyo, taarifa haikuweza kuanisha kuwa idadi ya wafungwa  wa Ukraine  walioachiliwa walikuwa  zaidi ya 150. SOMA: Vita ya Urusi ‘ilivyomhamishia’ raia wa Ukraine kijijini Kizimkazi-Unguja  

Utaratibu huu wa kubadilishana wafungwa kati ya Urusi na Ukraine  umekuwa ukifanyika katika  kipindi cha miaka mitatu tangu kuanza kwa vita vyao.

Urusi imesema askari wake kwanza walipelekwa kwenye mpaka wa jirani yake Belarus, ambako walipewa msaada wa kisaikolojia na matibabu kabla ya kupelekwa Urusi.