Vijana 100 wanufaika FDC Sikonge

SERIKALI chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan imeendelea kuleta mabadiliko chanya kupitia elimu ya ufundi stadi. Mafanikio hayo yanaonekana katika Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Sikonge kilichopo Tabora, ambapo takriban vijana 100 wamepata mafunzo ya fani mbalimbali ikiwemo umeme, ushonaji, uchomeleaji na ufundi bomba.

Kwa mujibu wa Mkuu wa chuo hicho, Gaston Chiwalanga, hatua hiyo imewezekana baada ya serikali kutoa shilingi milioni 50 kugharamia mafunzo hayo.Mbali na elimu, vijana hao pia wanapatiwa huduma muhimu kama chakula na malazi bure, jambo linalowawezesha kujikita kikamilifu katika kujifunza na kujenga mustakabali wao.

Mpango huu umeleta matumaini mapya kwa vijana wengi waliokuwa na changamoto za kifedha, na sasa unawapa nafasi ya kujitegemea na kushiriki katika kukuza uchumi wao binafsi pamoja na taifa kwa ujumla. SOMA : Wafungwa 73 wahitimu mafunzo ufundi stadi

Habari Zifananazo

2 Comments

  1. JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 12000-16700 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..
    .
    This is my main concern…………………… http://Www.Cash54.Com

  2. I just came across this amazing way to earn $11,000-$15,000 a month online! No selling, no struggle—just a simple system that anyone can follow. Mia Westbrook did it, and so can you! Don’t miss out on this life-changing opportunity.
    .
    This is what I do…………………… http://Www.Payathome9.Com

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button