Wahudumu afya wapatiwa chanjo kudhibiti Ebola

SIERRA LEONE : WAZIRI  wa Afya nchini Sierra Leone, Austin Demby  amesema serikali imezindua kampeni ya chanjo ya kitaifa dhidi ya ugonjwa wa Ebola kwa wafanyakazi wa afya baada ya mlipuko wa ugonjwa kutokea katika nchi hiyo.

Demby amesema  chanjo hizo zitawafikia wahudumu wa afya 20,000 ambao watapatiwa  chanjo hiyo.

Aidha amesema wahudumu wa afya ni kundi ambalo linakabiliwa na hatari ya maambukizi kabla ya kuwafikia wagonjwa kadhalika na madereva wanaobeba  wagonjwa wa Ebola.

Advertisement

Kundi lingine ambalo litapatiwa  chanjo ni kundi la waganga wa kienyeji na washauri  ambao mara nyingi  wa kwanza kuwasiliana na wagonjwa.

Demby  ameongezea kuwa  utoaji wa chanjo hiyo ya Ebola utaweza kulinda vyema mfumo wa huduma ya afya na wafanyakazi wake dhidi ya ugonjwa huo ili kupunguza madhara ndani ya jamii. SOMA : Virusi vya Ebola hukaa kwenye mbegu za kiume