‘Wakuu wa Mikoa saidieni utoaji haki’

JAJI Mkuu wa Tanzania Profesa Ibrahim Juma, amewataka wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya nchini kujua muundo na utendaji wa mahakama nchini, ili kusaidia kukabili changamoto zinazojitokeza katika mchakato mzima wa kusimamia na kutoa haki wa mahakama.
Jaji Mkuu amesema hayo mkoani Kigoma, akifungua mkutano wa Tume ya Utumishi ya mahakama na Kamati za Maadili za Mahakama za Mkoa Kigoma na wilaya zake na kubainisha kuwa, viongozi hao wana nafasi kubwa katika kushughulikia changamoto zinazojitokeza katika utoaji haki.
Profesa Juma amesema kuwa ukosefu wa mahakama katika baadhi ya wilaya nchini unachangia kuchelewesha utoaji haki katika mahakama nchini, hivyo wakuu wa mikoa na wilaya wanayo nafasi kubwa ya kuzungumzia jambo hilo kwa mamlaka mbalimbali, serikali na wadau wa maendeleo sambamba na kusimamia utekelezaji wake.
Pia Jaji Mkuu alitolea mfano wa ukosefu wa mkongo wa Taifa katika baadhi ya wilaya, ambao umesababisha utekelezaji wa mpango wa uendeshaji wa mashauri kwa njia ya video almaarufu mahakama mtandao kukwama na hivyo kuchelewesha utoaji haki.
Make money online from home extra cash more than $18000 to $21000. Start getting paid every month Thousands Dollars online. I have received $26000 in this month by just working online from home in my part time. every person easily do this job by.
…
Just Open This Website………>>> http://www.Richcash1.com