Waliokufa mafuriko Somalia wafikia 29

SOMALIA: IDADI ya watu waliokufa kutokana na mafuriko yanayoendelea nchini Somalia imefikia 29, Shirika la Kitaifa la Kukabiliana na Majanga (SOMDA) limeeleza.

Taarifa iliyonukuliwa na Reuters kutoka katika shirika hilo imefafanua zaidi ya watu 300,000 wamelazimika kukimbia makazi yao kutokana na ghasia hiyo.

Mapema wiki hii, Somalia ilitangaza hali ya dharura katika majimbo yaliyoathirika zaidi ya Jubbaland, Hirshabelle Kusini Magharibi na Galmudug.

Mafuriko hayo yalianza mwezi uliopita baada ya mvua kubwa iliyonyesha kuongeza kiwango cha maji na kusababaisha mafuriko katika mito ya Juba na Shabelle.

“Kinachoendelea leo ni kibaya zaidi kwa miongo kadhaa. Ni mbaya zaidi kuliko hata mafuriko ya 1997,” alisema Hassan Isse, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo (SOMDA).

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button