Wanafunzi 100 kutofanya mtihani kidato cha 4

Wazazi walaumiwa kwa ‘fake life’

DAR ES SALAAM: WANAFUNZI zaidi ya 100 wa shule huria ya Ukonga Skillful hawatafanya mtihani wa kidato cha nne utakaoanza Novemba 13, 2023 kutokana na sababu mbali mbali ikiwemo utoro.

Hayo yamesemwa Diodorus Tabaro katika mahafali ya 17 ya shule hiyo iliyopo Ukonga jijini Dar es Salaam.

Amesema, changamoto kubwa ambayo wamekuwa wakikabiliana nayo ni mdondoko wa wanafunzi ambao wamekuwa wakiacha shule kutokana na changamoto za kifamilia na tabia rika.

“Mdondoko wa wanafunzi unasababishwa na utoro, tabia rika, maisha magumu ya shule yanawakatisha tamaa, wengine wanakimbia kwa kuwa shule kuna sheria kali zinazowabana wakati wao wanataka kuwa huru”amesema.

Amesema, pia tatizo kubwa la shule huria hawana uwezo wa kuwabana mwanafunzi kuendelea kusoma na kwamba wamechukua maana ya huria kwenye maisha halisi.

“Kuna wanafunzi wanakuja kujisajili ndani ya mwezi mmoja haonekani, na wengine wanakuja kujisajili shule bila kuwataarifa wazazi au walezi na matokeo yake wanakosa wa kuwalipia ada wanaacha”amesema.

Tabaro pia ametoa lawama kwa wazazi ambao wamekuwa wakiishi na kuwalea watoto wao maisha ya kuigiza ‘Fake life’ ambayo uwaathiri watoto hata katika maisha yao ya kitaaluma.

“Wazazi wengi tumezaliwa maisha ya kawaida, lakinii ndani ya vichwa vya wazazi ni kutamani mtoto wake aishi maisha ya ‘standard’ ya juu, maisha ambayo hata kudeki mtoto hajui dada wa kazi ndio afanye, shuleni asifanye kazi, akitaka kitu fulani anapatiwa, mtoto anaweza kusema leo siendi kanisani, siendi msikitini mzazi anaona kawaida tu.

“Mtoto wa Sekondari anamiliki simu, anaingia mitandao ya Instagram, Facebook, TikTok, maisha ya huko kwenye mitandao sio maisha halisi, lakini wazazi ufurahi na kupenda na ujivunia kuona mtoto wake anatumia mitandao, tumesahau uhalisia.”amesema na kuongeza

“Lakini tunaposema ‘fake life’ hata shuguli ndogo za nyumbani hawezi, kumuachia familia kama wadogo zake kijana wa miaka 15 au 17 hawawezi kuwahudumia, maisha hayo yanawafuata mpaka kwenye maisha yao ya kitaalum;…. “mwanafunzi akipata kihoma kidogo tu unasikia naomba mpigie simu mami, mpigie dad, akimpigia analia na mzazi anaona ni jambo la kutisha, tunapaswa kuishi maisha ya uhalisia”alisisitiza Tabaro.

Naye Diwani wa Ukonga Ramadhani Bendera alihisii jamii kushirikiana na walimu katika malezi ili kujenga watoto wenye maadili mema.

Amesema Kata ya Ukonga imeunda kamati maalum ya kushughulika na changamoto za watoto wote wa Ukonga ikisimamiwa na Mtendaji wa Kata hiyo.

“Tabia rika sisi kama serikali tunapambana kuziondoa, tushirikiane tuziondoe kuanzia majumbani mwetu, kama serikali tutafanya kwa upande wetu, wazazi na jamii kwa ujumla nao watusaidie kwa upande wao, tutakuwa tunahudumia mashuleni na nyie wazazi muwahudumie majumbani. Mtoto alelewi na mzazi peke yake au mwalimu peke yake ni wa jamii nzima” amesema.

Awali, akisoma risala ya wanafunzi, mwanafunzi Debora Koroso alisema baadhi ya wazazi wanajisahau na hawafuatilii mienendo ya watoto wao na kujikuta wanajiingia kwenye tabia mbovu za uhuni, ulevi na kupelekea watoto kuanguka kitaaluma na wengine kuacha shule.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Julia
Julia
27 days ago

Mike, great work. I applaud your efforts enormously because I presently make more than $36,000 each month from just one straightforward online company! You may begin creating a steady online income with as little as $29,000, and these are only the most basic internet operations jobs.
.
.
Detail Here——————————————————–>>>  http://Www.BizWork1.Com

StaceyCanales
StaceyCanales
27 days ago

I’ve gained only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, mtg I was very troubled and thankfully
following website___________ http://Www.Careers12.com

Last edited 27 days ago by StaceyCanales
Back to top button
2
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x