DAR ES SALAAM:Askari wa jeshi la polisi waliotimiza miaka tisa kazini depo ya mwaka 2013/2014 (H3) wametoa msaada wa taulo za wanafunzi wa kike shuleni.
Hatua hiyo ni baada ya askari wa jeshi hilo kuguswa na kampeni ya namthamini inayoendeshwa na kituo cha Televisheni na Redio cha East Afrika ambacho kinalenga kuwasaidia watoto wa kike walioko shuleni.
Akizungumza mara baada ya kukabidhi taulo hizo, mkufunzi wa Chuo cha Taaluma ya Polisi Daer es salaam (DPA) ambaye aliambatana na askari hao Mkaguzi wa Jeshi la Polisi INSP, Lule Mlay amebainisha askari hao wameungana kumshukuru Mungu kwa kufikia miaka hiyo ya utumishi ndani ya jeshi hilo.
Kwa upande wake mwanafunzi wa kozi ya mkaguzi msaidizi wa polisi, Digna Miho amesema wameamua kumshukuru Mungu kwa kulikumbuka kundi la mabinti waliopo mashuleni huku akibainisha kuwa anafahamu changamoto za mabinti wanapokuwa katika mizunguko ya mwezi.