Wanafunzi wanne waliopata mimba warudi darasani

WANAFUNZI wanne kati ya 19 waliopata ujauzito wakiwa shuleni katika Halmashauri ya Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro, wamerejea kuendelea na masomo yao baada ya kujifungua.
Kurejea kwao shuleni ni utekelezaji wa mwongozo wa kuwarejesha shuleni wanafunzi waliokatiza masomo katika elimu ya msingi na sekondari kutokana na sababu mbalimbali, ambao ulitolewa Februari mwaka jana na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia.
Mwongozo huo unatekeleza tamko la kisera la serikali lililotolewa Novemba 2021 kuwaruhusu wanafunzi waliopata ujauzito kurejea katika mfumo wa elimu rasmi baada ya kujifungua.
Ofisa Elimu wa Sekondari katika Halmashauri ya Moshi, Benedict Sandy aliliambia HabariLEO kuwa wanafunzi waliorejeshwa shuleni kuendelea na masomo ni wale walioacha shule mwaka jana na mwaka juzi, wamerudi shuleni mwaka huu kuendelea na masomo yao.
“Wanafunzi waliorudi shuleni mwaka huu, wawili wapo kidato cha tatu na hao wengine wawili ni wa kidato cha nne na wanasoma katika shule za sekondari za Darajani, Mruwia, Cyril Chami na Uparo,” alisema.
“Kidato cha kwanza alikuwapo mwanafunzi mmoja wa shule ya Komakya aliyepata ujeuzito, kidato cha pili mmoja wa Shule ya Lyakirimu, kidato cha tatu wanafunzi tisa kutoka shule za Kimochi, Kirima, Manushi Day, Masoka, Mbokomu, Mpirani, Kilimani, Ghona na Rukima na kidato cha nne ni katika shule za Mboni, Kisuluni, Mruwia, Mangi Marealle, Mashingia, Sakayo Mosha na Uparo na Kidato cha Sita ni Weruweru,” alisema.
Mwongozo wa kuwarejesha shuleni wanafunzi walioacha shule kwa sababu mbalimbali, unatoa hadi miaka miwili ya kurejea shuleni kwa mwanafunzi aliyekatiza masomo kutokana na ujauzito, ukitoa fursa muhusika kumlea mtoto katika miezi yake ya awali ya makuzi.
Kabla ya kumrejesha mwanafunzi, mwongozo unataka uongozi wa shule kuitisha kikao cha pamoja baina ya mzazi ama mlezi na kamati ama bodi ya shule kujadili namna ya kumsaidia mwanafunzi husika. Pia unaelekeza mwanafunzi kurejea shuleni mwanzo wa mwaka mpya wa masomo katika darasa alilokatiza masomo.
“Kupewa huduma ya ushauri unasihi, hairuhusiwi kwa mwanafunzi aliyerejea shuleni baada ya kujifungua kwenda shuleni na mtoto wake,” unaeleza muongozo huo. Kadhalika mwongozo huo unaeleza kuwa unatoa wajibu kwa Ofisa Elimu Msingi ama Sekondari kutoa elimu kuhusu urejeshwaji wa wanafunzi waliokatiza masomo, suala ambalo Sandy alisema baada ya kupata mwongozo huo Februari waliwaita wakuu wa shule na maofisa elimu kata kuwapa elimu husika.
Alisema muongozo ulieleza wazi kwamba mwanafunzi anaweza akarudi kwenye shule ile ile aliyokua akisoma awali au akaamua kwenda kwenye shule nyingine atakayopenda au itakayoamuliwa na wazazi au walezi kwa kushauriana na na yeye mwenyewe.
“Kwa hiyo wanafunzi wanapotaka kurudi shuleni asilimia kubwa wamekuwa wakiomba wabadilishiwe shule. Kwamba alikuwa anasoma Sekondari ya Darajani, sasa anataka apelekwe labda Sekondari ya Marangu,” alisema
Make extra profit every week… this is a great part-time job for everyone… best part about it is that you can work from your home and earn from $100-$2000 each week … start today and have your first payment at the end of the week.
This Website➤—————➤ http://Www.Smartcash1.com
I’ve gained only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, mtg I was very troubled and thankfully
following website___________ http://Www.Careers12.com
I’m making a good salary from home 16,580-47,065/ Dollars week, which is amazing under a year ago I was jobless in a horrible economy. I was blessed with these instructions and now it’s my duty to pay it forward and share it with everyone.
.
.
Detail Here————————————————————–>>> http://Www.BizWork1.Com
★I am making a real GOOD MONEY (123$ / hr ) online from my laptop. Last month I GOT check of nearly $30k, this online work is simple and straight forward, don’t have to go OFFICE, Its home online job.(nja) You become independent after joining this JOB. I really thanks to my FRIEND who refer me this SITE. I hope you also got what I…go to home media tech tab for more detail reinforce your heart…
══════HERE► http://Www.Smartcareer1.com
Google paid 99 dollars an hour on the internet. Everything I did was basic Οnline w0rk from comfort at hΟme for 5-7 hours per day that I g0t from this office I f0und over the web and they paid me 100 dollars each hour. For more details
visit this article————>> http://simplwork36.blogspot.com