Watu 20 wauawa Lebanon

LEBANON : TAKRIBAN watu 20 wamewawa na 450 kujeruhiwa katika duru mpya ya milipuko nchini Lebanon, ambapo milipuko hiyo ikitokea kwenye redio za mawasiliano zilizolipuliwa kwa mbali ambazo hutumiwa na wanamgambo wa Hezbollah.
Shambulio hilo la pili nchini Lebanon ambalo limesababisha vifaa vya mawasiliano vya mkononi kama simu kulipuka.
Septemba 18, vifaa vya mawasiliano ya ujumbe vya pager vililipuka na kuwauwa watu 12, wakiwemo watoto wawili, na kuwajeruhi wengine takribani3,000.
Vyanzo kadhaa vimeelezea kuwa Israel iliwalenga washambuliaji wa Hezbollah.
Hezbollah inalaumu mashambulio yamefanywa na Israel, ambayo haijasema lolote licha ya wataalam wa usalama wa mashariki ya kati na Marekani kuviambia vyombo vya habari vya Marekani kwamba mashambulizi ya Jumanne yalifanywa Mossad, ambayo ni idara ya ujasusi ya Israel.
Licha ya kuwepo na malalamiko dhidi yao Israel wamesema leo inafungua awamu mpya katika vita na wanajeshi wake wakihamia upande wa kaskazini wa eneo la Lebanon.
SOMA : Watu Tisa wapoteza maisha Lebanon
Chanzo cha habari kutoka BBC kimethibitisha kikosi cha 98 cha jeshi la Israel kimehamia kutoka Gaza hadi kaskazini mwa Israel.



