Watu 80 wafa ajali ya moto Hawaii

IDADI ya watu waliokufa kwa ajali ya moto katika msitu wa Maui Hawaii imeongezea na kufikia 80.

Mwanasheria Mkuu wa Hawaii alisema Ijumaa kwamba alikuwa akifungua uchunguzi jinsi mamlaka iza uokozi zilivyowajibika, ambapo licha ya vifo hivyo watu 1,418 wamepoteza makazi kulingana na tawimu.

“Idara ya Mwanasheria Mkuu itafanya mapitio ya kina ya maamuzi muhimu na sera za kudumu zinazoongoza, wakati, na baada ya moto wa kwenye visiwa vya Maui na Hawaii wiki hii,” ofisi ya Mwanasheria Mkuu Anne Lopez ilisema. katika taarifa yake.

Moto huo umekuwa mbaya zaidi katika historia ya Hawaii, ukipita ile ya Tsunami iliyoua watu 61 kwenye kisiwa kikubwa cha Hawaii mnamo 1960.

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button