Waziri aagiza mgodi uanze uzalishaji

WAZIRI wa  Madini Doto Biteko, ametaka uongozi wa mgodi  wa Kampuni ya Williamson Diamond  LTD uliopo Mwadui wilayani  Kishapu mkoani Shinyanga,  kuanza kazi ya uzalishaji wa madini ya almasi Julai 15, 2023 baada ya kusitisha uzalishaji takribani miezi sita tangu bwawa la maji tope libomoke.

Biteko ameyasema hayo Juni 30, 2023, baada ya kufanya ziara  ya kutembelea bwawa la maji tope jipya likiwa na ukubwa wa hekta 57.2 litakalodumu kwa muda wa miaka miwili nusu.

Biteko amesema  uzalishaji uanze tarehe hiyo na kibali watapewa Jumanne wiki ijayo kwenye ofisi ya Mhandisi  mkuu  na kibali cha watu wa  bonde la maji kitashughulikiwa.

“Ninawapongeza uongozi wa mgodi huu, serikali ya mkoa na wilaya kwa ushirikiano  mzuri mliouonesha, kwani mlisimama hakuna siasa iliyoingizwa na kila mwananchi aliyeathirika kupata haki yake, “alisema Biteko.

Mhandisi  Henry Nditi Mkaguzi  Mkuu kutoka Tume ya Madini, amemueleza Waziri  Biteko  kibali kipo muda wowote watakapohitaji, kwani bwawa hilo limeonekana kukamilika kiasi kikubwa.

Mkuu wa Wilaya ya Kishapu,  Modest Mkude amesema makubaliano yalifanyika siku tatu zilizopita  na uongozi wa mgodi wapate kibali na kuanza uzalishaji hakuna mgogoro wowote hali ni shwari na asilimia 96 wameshalipwa  fidia kwa  walioathirika na tope hapo awali.

Mbunge wa Jimbo la Kishapu Boniface Butondo,  ameishukuru serikali kuchukua hatua na kulisimamia suala hili ambalo limeenda vizuri, kwani mgodi huo umesaidia kunyanyua uchumi wananchi  wa wilaya kwa kulipa mapato na kutoa ajira.

Meneja Mkuu wa Mgodi wa Almasi Mwadui, Ayoub  Mwenda amesema wao wako tayari kuanza uzalishaji kuanzia wiki ijayo wanachosubiri ni kibali kutoka ofisi za Madini,  kwani bwawa hilo limekamilika na mitambo iko vizuri.

Mhandisi Anael Macha kutoka kampuni ya City Engineering amesema bwawa hilo lilianza kutengenezwa mwezi March mwaka huu na Sasa limekamilika litaweza kudumu kwa muda wa miaka miwili na nusu lina ukubwa wa hekta 57.2

 

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Mining Census 2023
Mining Census 2023
1 month ago

Mining Census 2023

Watanzania mnakaribishwa kwenye SENSA ya Madini 2023 yenye lengo la kujua idadi ya migodi Tanzania, Idadi ya wachimbaji au watanzania wanaoshughulika na sekta ya Madini, Hali ya uchimbaji wa madini (zana zitumikazo kwa kila mgodi) na mapendekezo ya mbinu za kuboresha Sekta ya Madini.

Back to top button
1
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x