Yametimia Daraja la JP Magufuli

MWANZA; Taswira ya Daraja la J.P Magufuli (Kigongo-Busisi) lenye urefu wa km 3.0 pamoja na barabara unganishi zenye urefu wa km 1.66 ambalo limefunguliwa rasmi na Rais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan katika eneo la Kigongo, Misungwi mkoani Mwanza leo Juni 19, 2025.
Daraja hilo ambalo ni sehemu ya barabara ya Usagara-Sengerema-Geita ni sehemu ya barabara kuu inayoanzia Sirari hadi Mtukula na ujenzi wake ulianza rasmi mwezi Februari, 2020.