Mtoto ajinyonga kisa kukanywa na wazazi

POLISI mkoani Morogoro wanachunguza kifo cha Rajabu Ally Mohammed (12), mtoto wa nyumbani na mkazi wa Ijava, Kata ya Italagwe, Wilaya ya Gairo aliyekutwa amejinyonga nyuma ya nyumba yao kwa kutumia mkanda wa suruali.
Kamanda wa Polisi wa mkoa huo, Alex Mkama amesema tukio hilo lilitokea asubuhi ya Machi 23, 2026, katika Kitongoji cha Kaloleni, Kata ya Italagwe. Uchunguzi wa awali umebaini kuwa siku ya Machi 22, Rajabu alikemewa na wazazi wake kuacha vitendo vya udokozi baada ya kukamatwa akiwa na wenzake wawili wakiwa wameiba mahindi mabichi.
Kamanda Mkama amesema kitendo cha kukemewa kilimjaza hasira na kumfanya mtoto huyo kujiua. Kufuatia tukio hilo, Kamanda Alex amewataka watoto wote mkoani humo kusikiliza mafundisho ya wazazi, walimu na viongozi wa kijamii ili kuepuka tabia mbaya zitakazoweza kuwapelekea kupoteza maisha. SOMA: Binti darasa la nne adaiwa kujinyonga




JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 12000-16700 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..
.
This is my main concern…………………… http://Www.Cash54.Com
I just came across this amazing way to earn $11,000-$15,000 a month online! No selling, no struggle—just a simple system that anyone can follow. Mia Westbrook did it, and so can you! Don’t miss out on this life-changing opportunity.
.
This is what I do…………………… http://Www.Payathome9.Com