DC Kondoa awasihi wananchi kujitokeza kupiga kura Oktoba 29

KONDOA: MKUU wa Wilaya ya Kondoa, Fatma Nyangasa, amewasihi wananchi wa wilaya hiyo kujitokeza kwa wingi kushiriki Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025. Akizungumza katika ziara ya Kata ya Serya, Nyangasa alisema wananchi wanapaswa kutumia haki yao ya kuchagua rais, wabunge na madiwani.
Alitumia ziara hiyo pia kusikiliza kero za wananchi zikiwemo changamoto za daraja la Mto Bubu, ukosefu wa umeme katika Kituo cha Afya Serya, eneo la malisho na upatikanaji wa maji. Nyangasa alisema tayari amewasilisha baadhi ya changamoto hizo kwa mamlaka husika na ataendelea kufuatilia utekelezaji wake.SOMA: Viongozi wapewa mbinu kumaliza kero za wananchi



