Yanga yatota Malawi

MALAWI; Yanga ya Dar es Salaam imekubali kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa Silver Strikers ya Malawi katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika uliofanyika leo nchini Malawi.

Yanga ili isonge mbele na kutinga hatua ya makundi italazimika kushinda kuanzia mabao 2-0 katika mchezo wa marudiano wiki ijayo Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam. (Picha kwa hisani ya Yanga).




