watendaji vituo vya kura washauriwa kupitia sheria

MTWARA: WATENDAJI wa vituo vya kupigia kura katika Jimbo la Tandahimba mkoani Mtwara wametakiwa kusoma kwa umakini katiba, sheria na kanuni wakati wa utekelezaji wa majukumu hayo.
Ushauri huo umetolewa leo Oktoba 26, katika mafunzo ya siku mbili yaliyohusisha na kiapo cha kujitoa uwanachama na kutunza siri kwa watendaji hao wa vituo hivyo yaliyofanyika kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba mkoani humo kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025.

Akifungua mafunzo hayo, Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi Jimbo la Tandahimba Ramadhani Mmbughu amesema mafunzo hayo yamehusisha watendaji hao 1771 wakiwemo wasimamizi wa vituo na wasimamizi wasaidizi wa vituo wataofanya shughuli za uchaguzi katika vituo 569 vilivyopo kwenye kata 32 za halmashauri hiyo.
Aidha mafunzo hayo yana lengo la kubadilishana uzoefu na kujadiliana namna ya kufanikisha uchaguzi huo katika maeneo yao pia kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazoweza kujitokeza katika hatua mbalimbali za zoezi hilo la kupiga na kuhesabu kura.

“Uchaguzi ni mchakato unaojumuisha hatua na taratibu mbalimbali za kikatiba na sheria ambazo hupaswa kufuatwa na kuzingatiwa hasa katika ngazi ya kituo,”amesema Mmbughu
Aidha ametumia nafasi hiyo kuwaasa watendaji hao kuwa pamoja na uzoefu ambao baadhi yao wanao katika uendeshaji wa uchaguzi ila wasiache kusoma katiba, sheria na kanuni zinazotolewa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC).

“Someni kwa umakini katiba, sheria, kanuni, miongozo na maelekezo mbalimbali yaliyotolewa na yatakayotolewa na Tume na ulizeni ili mpate kufafanuliwa kwenye maeneo ambayo kwa namna moja au nyingine pengine yatakuwa na changamoto za kufahamu,”amesisitiza Mmbughu
Sambamba na hilo miongoni mwa majukumu na wajibu wa watendaji hao wakati wa zoezi hilo ikiwemo kuzingatia muda wa kuripoti eneo la kituo cha kupigia kura ili kuepusha migogoro isiyo ya lazima wakati wa zoezi hilo na mengine.





JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 6000-12700 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..
.
This is my main concern……………………………………. http://Www.Cash43.Com
Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
.
More Details For Us→→→→→→→→→→ http://Www.Payathome9.Com