Kituo cha kupozea umeme Nyakanazi kupanuliwa

GEITA: SERIKALI kupitia Wizara ya Nishati imepanga kufanya upanuzi wa kituo cha kupoza umeme Nyakanazi kilichopo wilayani Biharamulo ili kuunganisha mfumo wa gridi ya taifa na kutanua uwigo wa huduma ya umeme.

Mpango huo unalenga kutengeneze mfumo ambao utaunganisha gridi yote ya taifa ndani nchi ya Tanzania na kuunda mfumo mmoja uliounganishwa na kuliwezesha taifa kuuza umeme nje ya nchi.

Mhandisi Msimamizi wa Kituo cha Kupoza Umeme Nyakanazi, Mhandisi Isack Kisandu ametoa taarifa hiyo mbele ya waandishi wa habari mkoani Geita walipofanya ziara maalum kutembelea kituo hicho.

Amesema mpaka sasa kituo hicho kina njia kuu tatu ambazo zote zina uwezo wa Kilovati 220 ambapo upanuzi ukikamilika utaongeza kiwango cha umeme kwenye kila njia hadi kufikia Kilovati 400.

“Laini moja inapokea umeme kutoka Geita ambayo ina umeme wa gridi ya taifa, laini ya pili inapokea umeme kutoka kituoz cha kufua umeme cha Rusumo na laini ya tatu inapeleka umeme Kigoma.

“Tunataka kupanua kituo kwa ajili ya kuunganisha gridi nzima ya taifa kwani kuna maeneo mengine kama Sumbawanga ambao wanapata umeme kutokea nchini Zambia”, amesema Mhandisi Kisandu.

Amesema kituo kina mashine umba (transifoma) mbili zenye uwezo wa 40 MVA kila moja ambazo zinasaidia kupunguza kiwango cha voltage kutoka Kilovoti 220 kwenda 33 Kilovoti kwa ajili ya matumizi.

Amesema pia kituo cha Nyakanazi kina mashine vilishio (feeder) kuu nne ambazo zinalisha kwenye wilaya saba zilizopo kwenye mikoa mitatu tofauti nchini.

“Kwa mkoa wa Kagera tunalisha wilaya ya Ngara na Biharamulo, kwa mkoa wa Geita tunalisha wilaya ya Chato, Bukombe na Mbogwe huku kwa Kigoma kuna wilaya ya Kakonko na Kibondo.

“Tuna eneo kubwa sana la kupeleka umeme kwa ajili ya wananchi kwani kituo cha Nyakanazi ni kituo cha kwanza kinachpokea umeme kutoka kituo cha kufua umeme cha Rusumo”.

Amesema kituo cha Nyakanazi kinapokea wastani wa Megawati 27 kutoka Rusumo ambapo wilaya zinazopokea umeme kutoka hicho zinatumia takribani Megawati 19 na kusalia na ziada kwenye gridi.

Habari Zifananazo

3 Comments

  1. JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 6000-12700 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..

    .

    This is my main concern……………………………………. http://Www.Cash43.Com

  2. Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
    .
    M­­­­­­o­­­­­­r­­­­­­e­ D­­­­­­e­­­­­­t­­­­­­a­­­­­­i­­­­­­l­­­­­­s For Us→→→→→→→→→→ http://Www.Payathome9.Com

  3. I’ve gained $17,240 only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, I was very troubled and thankfully I’ve located this project now in this way I’m in a position to receive thousand USD directly from home. Each individual certainly can do this easy work & make more greenbacks online by
    visiting following website….>>> https://www.Homeprofit1.site

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button