SMZ yajipanga kuzuia usafirishaji wa binadamu

TAASISI zinazohusika na kuzuia na kupambana na usafirishaji haramu wa binadamu zimetakiwa kuongeza ubunifu na kutumia mbinu za kisasa kubaini vyanzo vyote vya uhalifu huo, ambao umeendelea kuwaathiri kwa kiwango kikubwa wanawake na watoto nchini.

Wito huo umetolewa leo, Novemba 26, 2025, na Mkurugenzi wa Uratibu wa Shughuli za Serikali, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Siajabu Suleiman Pandu, wakati akifungua Kikao cha Wadau wa Serikali cha kujadili namna ya kuimarisha ushirikiano katika mapambano dhidi ya usafirishaji haramu wa binadamu, kilichofanyika Mwembe Madema, Mkoa wa Mjini Magharibi.

Akizungumza katika kikao hicho, Pandu amesema jamii inapaswa kutoa taarifa za matukio yanayohusiana na usafirishaji haramu wa binadamu kwa vyombo vya dola ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa. “Vita dhidi ya usafirishaji haramu wa binadamu haiwezi kufanikiwa bila ushiriki wa wananchi. Taarifa sahihi kutoka kwa jamii ni msingi wa kuchukua hatua za haraka na madhubuti,” alisema.

Kwa upande wake, Afisa Mwandamizi wa Sekretarieti ya Kuzuia na Kupambana na Usafirishaji Haramu wa Binadamu, Rafii Said Mnete, amesema Serikali kupitia Sekretarieti hiyo imejipanga kuboresha mikakati na kuchukua hatua thabiti za kukabiliana na vitendo hivyo, ikiwemo kuimarisha ufuatiliaji, elimu kwa umma na ushirikiano wa taasisi. “Tunazidi kuongeza nguvu katika maeneo yote muhimu kuzuia, kutambua na kuchukua hatua. Huu ni uhalifu mtandao unaohitaji ushirikiano mpana,” alieleza.

Naye Naibu Katibu wa Sekretarieti hiyo, Kanda ya Zanzibar, Huzaimat Bakar Kheir, amesema lengo la kuzikutanisha taasisi hizo ni kuimarisha uratibu na kubadilishana taarifa ili kuongeza ufanisi katika kupambana na uhalifu wa usafirishaji haramu wa binadamu. “Ushirikiano wa taasisi ni silaha muhimu. Kupitia majadiliano haya tunaweka msingi wa hatua za pamoja zenye matokeo ya haraka,” alisema.

Kikao hicho kimehusisha taasisi mbalimbali za Serikali kutoka Zanzibar na Tanzania Bara, zikiwemo vyombo vya ulinzi na usalama, mamlaka za udhibiti, na idara za ustawi wa jamii. SOMA: Uhamiaji wakabidhiwa gari kudhibiti wahamiaji haramu

Habari Zifananazo

3 Comments

  1. JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 6000-12700 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..
    .
    This is my main concern……………………………………. http://Www.Cash43.Com

  2. Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
    .
    M­­­­­­o­­­­­­r­­­­­­e­ D­­­­­­e­­­­­­t­­­­­­a­­­­­­i­­­­­­l­­­­­­s For Us→→→→→→→→→→ http://Www.Payathome9.Com

  3. Google provides awesome remote work opportunities, allowing me to earn $2000-$3000 weekly with just 2-4 hours of daily work. It’s been a game-changer, offering flexibility and reliable income. If you’re seeking a genuine way to earn online, don’t miss this chance. Start today and transform your life!
    .
    More Details For Us →→ http://www.big.income9.com

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button