MWENYEKITI wa Ngome ya Vijana ya Chama cha ACT-Wazalendo, Abdul Nondo leo Oktoba 20 amejiandikisha katika daftari la mkazi kwa ajili ya kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 27 mwaka huu.
Kiongozi huyo amejiandikisha katika mtaa wa Livingstone, kata ya Kasingirima, jimbo la Kigoma Mjini, Mkoa wa Kigoma.
Katika mazungumzo yake mara baada ya zoezi hilo, Nondo amewahimiza vijana wote nchini ambao bado hawajajiandikisha kujitokeza na kufanya hivyo leo. Zoezi la uandikishaji linafikia tamati leo.
Mwenyekiti wa @NgomeyaVijana Taifa, Ndugu @abdulnondo2 amejitokeza kujiandikisha katika daftari la mkazi kwa ajili ya kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 27 mwaka huu
Nondo amejiandikisha katika mtaa wa Livingstone, kata ya Kasingirima, jimbo… pic.twitter.com/5b2bAnDE0H
— ACTWazalendo (@ACTwazalendo) October 20, 2024