Auawa akitaka kumshambulia paroko

MKAZI wa Kijiji cha Kagunguli wilayani Ukerewe mkoani Mwanza, Renatus Silivester ameuawa na wananchi baada ya kuingia ghafla katika Kanisa Katoliki wilayani Ukerewe kwa nia ya kumjeruhi paroko wakati waumini wakiendelea na Ibada ya Pasaka.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mwanza, Wilbrod Mutafungwa amesema tukio hilo lilitokea juzi asubuhi katika Parokia ya Kagunguli wilayani Ukerewe. Amesema kijana huyo anayesadikiwa kuwa na ugonjwa wa akili aliingia katika kanisa hilo kupitia mlango wa upande wa kulia akiwa amebeba mfuko na kuelekea moja kwa moja madhabahuni na mmoja wa waumini, alipomshtukia kutokana na mienendo yake alimtoa nje ya kanisa.

“Walipokuwa wakimhoji, kijana huyo alitoa upanga na kuwajeruhi watu wawili na kutokana na kitendo hicho, kundi la waumini na wananchi waliokuwa nje ya kanisa walimdhibiti kwa kumpiga kwa silaha za jadi na kumjeruhi sehemu mbalimbali za mwili wake,” alifafanua.

Hatahivyo, aliwataja waliojeruhiwa kuwa ni Costantine Bituro ambaye ni mwenyekiti wa Parokia na mkazi wa Kagunguli, aliyejeruhiwa kichwani na mikono yote na Aloyce Christopher ambaye ni mwanakwaya.SOMA: Ugomvi nyumbani, ugoni vyaongoza mauaji 2025

Kamanda Mutafungwa amesema kijana huyo alikimbizwa Hospitali ya Wilaya ya Nansio kwa ajili ya kupatiwa matibabu kutokana na majeraha aliyoyapata, lakini alifariki dunia kabla ya kufikishwa hospitalini.

Habari Zifananazo

3 Comments

  1. JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 12000-16700 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..
    .
    This is my main concern…………………… http://Www.Cash54.Com

  2. I just came across this amazing way to earn $11,000-$15,000 a month online! No selling, no struggle—just a simple system that anyone can follow. Mia Westbrook did it, and so can you! Don’t miss out on this life-changing opportunity……….
    .
    This is what I do…………………… http://Www.Payathome9.Com

  3. I believe what you posted made a great deal of sense.
    However, think on this, suppose you were to write a awesome title?
    I mean, I don’t want to tell you how to run your website, however suppose
    you added something that makes people desire more? I mean Auawa akitaka kumshambulia paroko – HabariLeo is a little boring.
    You should glance at Yahoo’s home page and watch how they create article headlines to grab people interested.
    You might add a related video or a related picture or two to get
    readers interested about what you’ve written. Just my opinion, it could make your posts a little bit more interesting.

    my site – sildenafil citrate 25mg

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button