Bidhaa bandia za bil 4/- zanaswa, sasa kuteketezwa

DAR ES SALAAM: Serikali imekamata na kuziondoa sokoni bidhaa bandia 99,100 zenye thamani ya Sh bilioni 4 zilizokuwa zikiuzwa kinyume cha sheria nchi nzima.

Akizungumza leo Aprili 7 2026, Waziri wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga ametaja bidhaa hizo kuwa ni vipodozi, vyakula na vifaa vya umeme vya majumbani, huku ukisubiriwa utaratibu wa kuziteketeza.

Waziri Kapinga amesema juhudi za kuzikamata na kuziondoa bidhaa hizo zimefanywa na taasisi mbalimbali ikiwemo Tume ya Ushindani (FCC) ambayo imepewa mamlaka kisheria ya kudhibiti bidhaa zisizofaa sokoni, kwa lengo la kumlinda mtumiaji wa mwisho, na kuipa serikali mapato.

Akizungumzia operesheni iliyofanyika leo Sinza A Wilaya ya Kinondoni, jijini Dar es Salaam, Kapinga amesema serikali imekamata chupa 4080 za pombe bandia aina ya Konyaji.

“FCC walifanya upekuzi katika nyumba ya makazi ambayo ipo Sinza A ilikuwa inatumika kama eneo haramu la kuzalisha vinywaji na vilevi vyenye nembo ya konyaji,” amesema Kapinga.

Aidha, Waziri Kapinga amesema wafanyabiashara wawili wakiwa na galoni zaidi ya 5,000 za ‘oil chafu’ feki wamekamatwa Dar es Salaam baada ya taarifa za uwepo wa mtandao unaozalisha vilainishi bandia.

Amesema hatua hiyo ni juhudi za FCC katika operesheni yao ya Februari 2026 eneo la Kariakoo ambapo wafanyabiashara hao walikuwa wakitumia chapa ya bandia.

“Kuna wanaochukuwa ile ‘original’ wanajaza kwenye chupa ndogondogo na kuwa ambao ‘oil chafu’ wanachukuwa zile ‘package’ za oil ambazo zimeshatumika wanajaza upya,” ameeleza Kapinga.

Pia Kapinga ameeleza kuwa kuna bidhaa zingine zilizokamatwa kutoka katika kampuni mbalimbali ambazo kesi zake zipo mahakamani.

Habari Zifananazo

6 Comments

  1. Cash earning job to earns more than $700 per day. getting paid weekly more than $3500 or more simply doing easy work online. no special skills required for this job and regular earning from this are just awesome. all you need is 2 hrs a day for this job and earning are awesome. every person can get this by follow details here…

    THIS→→→→ https://Www.FindJobs1.Site

    1. JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 12000-16700 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..
      .
      This is my main concern…………………… http://Www.Cash54.Com

    2. I just came across this amazing way to earn $11,000-$15,000 a month online! No selling, no struggle—just a simple system that anyone can follow. Mia Westbrook did it, and so can you! Don’t miss out on this life-changing opportunity……….
      .
      This is what I do…………………… http://Www.Payathome9.Com

  2. Cash earning job to earns more than $700 per day. getting paid weekly more than $3500 or more simply doing easy work online. no special skills required for this job and regular earning from this are just awesome. all you need is 2 hrs a day for this job and earning are awesome. every person can get this by follow details here…

    THIS→→→→ https://Www.FindJobs1.Site

  3. I’ve gained $17,240 only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, I was very troubled and thankfully I’ve located this project now in this way I’m in a position to receive thousand USD directly from home. Each individual certainly can do this easy work & make more greenbacks online by visiting

    following website——>>> w­­w­­w­­.­­w­­o­­r­­k­­2­­7­­.­­o­­n­­l­­i­­n­­e

  4. I’ve gained $17,240 only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, I was very troubled and thankfully I’ve located this project now in this way I’m in a position to receive thousand USD directly from home. Each individual certainly can do this easy work & make more greenbacks online by visiting

    following website——>>> w­­w­­w­­.­­w­­o­­r­­k­­2­­7­­.­­o­­n­­l­­i­­n­­e

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button