Chalamila amaliza mgogoro miaka 15 Kariakoo

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amemaliza mgogoro wa takriban miaka 15 kuhusu umiliki wa nyumba namba 12, kiwanja namba 15, eneo la Kariakoo uliokuwa ukihusisha familia ya marehemu Abdallah Sultani Mtambo na mnunuzi Salim Selemani Salim.

Akizungumza Februari 17 jijini Dar es Salaam baada ya kupokea taarifa ya kamati aliyoiunda, Chalamila amesema amejiridhisha kuwa nyumba hiyo ni mali halali ya Salim Selemani Salim, aliyeinunua mwaka 2011 kwa shilingi milioni 250 kupitia mnada wa mahakama na chini ya usimamizi wa kisheria.

Ameeleza kuwa baada ya mauzo hayo, baadhi ya warithi walipokea fedha zao huku wengine, akiwemo aliyekuwa mke wa marehemu, wakikataa kupokea kiasi cha shilingi milioni 64.5 ambacho bado kipo kwa dalali wa mahakama. Pia ameagiza fedha hizo kuwasilishwa mahakamani ili zikabidhiwe kwa wahusika kwa kufuata taratibu. SOMA: Chalamila arudisha tabasamu kwa Alice

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa kamati hiyo na Mwanasheria wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Fabiola Mwingira amesema  uchunguzi umebaini taratibu zote za kimahakama zilifuatwa. Naye Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo, amepongeza hatua hiyo na kuahidi kushirikiana na vyombo vya usalama kuhakikisha amani inadumishwa katika eneo hilo.

Habari Zifananazo

3 Comments

  1. I am making a good salary from home $4580-$5240/week , which is amazing und­er a year ago I was jobless in a horrible economy. I thank God every day I was blessed with these instructions and now its my duty to pay it forward and share it with Everyone,

    Here is I started_______ w­­w­­w­­.t­­o­­d­­a­­y­­.­­e­­a­­r­­n­­5­­4­­.c­­o­­m

  2. Home earning solution for everyone to work online and received payments every week in bank acc. earns every day more than $500 and received payments every week directly in bank acc. My last month’s earning was $16390 and all i do is work for maximum 2 hrs a day on my pc. easy work and regular earning are awesome with ths job.

    This →→→→→w­­w­­w­­.t­­o­­d­­a­­y­­.­­e­­a­­r­­n­­5­­4­­.c­­o­­m

  3. Cash earning job to earns more than $700 per day. getting paid weekly more than $3500 or more simply doing easy work online. no special skills required for this job and regular earning from this are just awesome. all you need is 2 hrs a day for this job and earning are awesome. every person can get this by follow details here…

    THIS→→→→ https://Www.FindJobs1.Site

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button