Chanjo ya mpox kuwasili Kongo

KONGO : SERIKALI ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo leo itapokea shehena ya kwanza ya dozi takribani 100,000 za chanjo ya Ugonjwa wa homa ya nyani Mpox.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia  ya Kongo kupitia Wizara ya Afya  imesema zoezi la utoaji wa chanjo utaanza kutolewa mwishoni mwa wiki hii .

Kituo cha kudhibiti na kuzuia magonjwa Afrika CDC, kimesema chanjo zingine laki 200,000 zinataraji  kuingia nchini Kongo kabla  ya mwisho wa wiki hii.

Advertisement

Seŕikali ya Kongo imepokea chanjo hizi kutoka kampuni ya dawa ya Bavarian Nordic iliyoko nchini Denmark.

SOMA : Afrika kunufaika na chanjo Mpox

Mpaka sasa zaidi ya wagonjwa 17,500  wamethibitika nchini Kongo kuwa wamepata virusi vya homa ya nyani  Mpox huku wengine 629  wakipoteza maisha kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani WHO.

SOMA : WHO : Afrika inaweza kutokomeza Mpox ndani ya miezi sita