Dulla Makabila aitwa Basata kuhusu wimbo Pita Huku

Baraza la Sanaa la Taifa (Basata, limemtaka msanii Abdallah Ahmed ‘Dullah Makabila’ kufika katika ofisi za baraza hilo kujadili wimbo wake mpya uitwao Pita Huku, ambao unaendelea kushika nafasi ya kwanza ‘Youtube’.

Taarifa ya kuitwa kwa msanii huyo imetolewa na Katibu Mtendaji wa Basata,  Dk Kedmon Mapana iliyosema: ‘Basata inapenda kuwajulisha kwamba kutakuwa na kikao kitakachofanyika tarehe 21/12/2022 siku ya Jumatano, ajenda ya kikao ni kujadili kuhusiana na wimbo wako wa Pita Huku”.-

Kupitia akaunti yake ya Instagram, Makabila amethibitisha kupokea barua hiyo: “Nimepokea barua ya wito kutoka Basata, ambayo inahusu wimbo wangu mpya wa Pita Huku, wito nimeupokea na nitafika leo nyie ni walezi wangu katika shughuli zangu za sanaa.-

“Mashabiki zangu asanteni Kwa kuufanya wimbo wetu wa Pita Huku kuwa trending number moja huko mjini Youtube, tuendelee kufuatilia kazi nzuri,”  ameongeza Makabila.

Habari Zifananazo

23 Comments

  1. Just saw the Pita Huku teaser and the fact it’s dropping on YouTube first is wild. Makabila’s team really pushed for the online hype—TikTok rulz. Hope the live discuss hits hard, but I’ll be vibing with the song either way.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button