Dulla Makabila aitwa Basata kuhusu wimbo Pita Huku

Baraza la Sanaa la Taifa (Basata, limemtaka msanii Abdallah Ahmed ‘Dullah Makabila’ kufika katika ofisi za baraza hilo kujadili wimbo wake mpya uitwao Pita Huku, ambao unaendelea kushika nafasi ya kwanza ‘Youtube’.

Taarifa ya kuitwa kwa msanii huyo imetolewa na Katibu Mtendaji wa Basata,  Dk Kedmon Mapana iliyosema: ‘Basata inapenda kuwajulisha kwamba kutakuwa na kikao kitakachofanyika tarehe 21/12/2022 siku ya Jumatano, ajenda ya kikao ni kujadili kuhusiana na wimbo wako wa Pita Huku”.-

Kupitia akaunti yake ya Instagram, Makabila amethibitisha kupokea barua hiyo: “Nimepokea barua ya wito kutoka Basata, ambayo inahusu wimbo wangu mpya wa Pita Huku, wito nimeupokea na nitafika leo nyie ni walezi wangu katika shughuli zangu za sanaa.-

“Mashabiki zangu asanteni Kwa kuufanya wimbo wetu wa Pita Huku kuwa trending number moja huko mjini Youtube, tuendelee kufuatilia kazi nzuri,”  ameongeza Makabila.

Habari Zifananazo

27 Comments

  1. Just saw the Pita Huku teaser and the fact it’s dropping on YouTube first is wild. Makabila’s team really pushed for the online hype—TikTok rulz. Hope the live discuss hits hard, but I’ll be vibing with the song either way.

  2. It’s always interesting to see how a song can stir up so much conversation, especially when it climbs to the top of YouTube like ‘Pita Huku’ has. The news about Basata calling in Dulla Makabila for a discussion makes me wonder what exactly they want to talk about—is it the lyrics, the message, or just the song’s popularity? I appreciate that the artist confirmed he received the letter and plans to attend; that shows a level of respect for the process. It feels like a moment where art and regulation are trying to find common ground, and I’m curious to see how it plays out. For anyone following the creative scene, this is a reminder that staying informed and engaged with the community matters. If you’re into tools that help you keep up with creative trends, you might find Vibe Coding Hub a handy resource.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button