EAC iungwe mkono kukamilisha sarafu ya pamoja

JUMUIYA ya Afrika Mashariki (EAC) imefanikiwa kusimamia vyema Itifaki ya Soko la Pamoja katika miaka 25 baada ya kuanzishwa tena mwaka 1999.
Kazi kubwa iliyopo mbele yake kuanzia 2025 ni kusimamia na kutekeleza sarafu ya pamoja, ikiwa ndiyo itifaki inayofuata kabla ya kuhitimisha na shirikisho la kisiasa.
Endapo itifaki ya sarafu ya pamoja itaridhiwa na nchi zote wanachama, kuna manufaa mengi yatakayopatikana ikiwa ni pamoja na biashara kufanyika bila kubadili sarafu mipakani.
Kwa mujibu wa Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, itifaki ya sarafu ya pamoja inatarajiwa kukamilika mwaka 2031, ikiwa nchi zote zitapitisha maazimio ya uundwaji wa sarafu hiyo.
SOMA: Kalonzo, Ngole wataka sarafu EAC iharakishwe
Tunaamini kuwa kutokana na mafanikio yaliyofikiwa katika utekelezaji wa itifaki ya soko la pamoja, vivyo hivyo utekelezaji wa itifaki ya sarafu ya pamoja utatimia, ikiwa kutakuwa na ushirikiano wa kutosha.
Hata hivyo, changamoto za mipakani kuhusiana na mazao na bidhaa zimepungua baada ya kuanza kutekelezwa na kusimamiwa vyema kwa itifaki hiyo, ambapo awali ilikuwa changamoto kubwa.
Kutokana na ushirikiano wa kiuchumi kuimarika zaidi katika Jumuiya ya Afrika Mashariki ambayo ndio jumuiya kongwe zaidi barani Afrika, inaelezwa kuwa hali hiyo inashajihishwa na usimamizi na utekelezaji mzuri wa Itifaki ya Soko la Pamoja miongoni mwa nchi wanachama.
Moja ya mafanikio makubwa ambayo kila mwananchi wa ndani ya jumuiya anaweza kujivunia waziwazi ni kupanuka kwa jumuiya kutoka nchi tatu za mwaka 1999 hadi kuwa nchi nane mwaka 2025.
Hayo ni mafanikio makubwa, kwa sababu yanaendelea kutafsiri maono ya waasisi wa jumuiya hiyo ambao ni Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere wa Tanzania, Mzee Jomo Kenyatta wa Kenya na Dk Milton Obote wa Uganda, ambao walilenga kuunganisha Bara la Afrika kupitia jumuiya zake.
Pamoja na mafanikio hayo, viongozi wa nchi za EAC wamefanikiwa kutekeleza itifaki mbili kati ya nne ambazo ni Umoja wa Forodha na Soko la Pamoja, ikiwa bado itifaki ya sarafu moja na Shirikisho la Kisiasa.
Mafanikio hayo yote ni katika kipindi hicho cha miaka 25 na maendeleo ya Sarafu ya Pamoja yanaenda vizuri, kwa sababu taarifa ya Sekretarieti ya EAC chini ya Katibu Mkuu, Veronica Nduva ilisema hadi kufika 2031 itakuwa imekamilika.
Kutekelezwa kwa itifaki ya soko la pamoja na Umoja wa Forodha kumesaidia kuanzishwa miradi mikubwa ya kimkakati ndani ya EAC kama Mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi (EACOP) kutoka Hoima nchini Uganda hadi Chongoleani, mkoani Tanga na mradi wa barabara za EAC.
Tunaamini kama viongozi wa nchi wanachama wa EAC wataendelea kujituma na kujitolea kuhakikisha itifaki zilizobaki zinatekelezwa, EAC inakuwa ya kwanza duniani kwa kuwa na nguvu na inayoamua mambo yake yenyewe.
Kuna kazi kubwa imefanyika kusaidia nchi zenye changamoto ya machafuko kama Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Sudan Kusini na Somalia, ili kuleta amani ya kudumu kwa njia ya mazungumzo na kwa njia ya kijeshi.
Tunaisihi Sekretarieti ya EAC pamoja na wakuu wa nchi kupitisha mapendekezo ya uundwaji wa sarafu ya pamoja kuwezesha wananchi kufanya biashara bila kulazimika kubadili fedha.
I get paid over (90$ to 500$ / hour ) working from home with 2 kids at home. I never thought I would be able to do it but my best friend earns over $22000 a month doing this and she convinced me to try. it was all true and has totally changed my life… This is what I do, check it out by Visiting Following web….
.
HERE——————————————⊃⫸ http://Www.Cash43.Com
Every month, I earn over $21,000 doing an online job from home in my spare time. Last month, I earned $19,685 from this simple internet business by working just 3 hours a day on my laptop. This work-from-home opportunity is incredible, and the daily earnings far exceed those of typical 9-to-5 desk jobs. Anyone can start earning money online by following the instructions on this website…
Open this… http://Www.Work99.Site
Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
.
More Details For Us→→→→→→→→→→ http://Www.Payathome9.Com
Every month start earning more than $12,000 by doing very simple Online job from home.i m doing this job in my part time i have earned and received $12429 last month .I am now a good Online earner and earns enough cash for my needs. Every person can get this Online
job pop over here this site… https://Www.Salary7.Zone
I am making a real GOOD MONEY (80$ to 92$ / hr. )online from my laptop. Last month I GOT a check of nearly 21,000$, this online work is simple and straightforward, I don’t have to go to the OFFICE. At that point this work opportunity is for you. If you are interested. Simply give it a shot on the accompanying site link… https://Www.EarnApp1.Com