Israel yashambulia ngome za Hezbollah

BEIRUT : ISRAEL imefanya mashambulizi mengine manne  ya anga  katika eneo la kusini  mwa mji wa Beirut  baada ya jeshi hilo kuwahimiza watu waondoke katika ngome ya Hezbollah .

Kwa mujibu wa Shirika la habari nchini humo -NNA limeripoti kutokea kwa mashambulizi hayo ambayo yalitokea katika maeneo  tofauti ikiwemo maeneo ya kusini katika eneo la Saint Therese na mashambulizi mengine  yakipigwa huko Burj al-Barajneh.

SOMA : Jeshi la Israel laingia Lebanon

Advertisement

Hatahivyo, Kikosi cha Kijeshi cha Israel -IDF kimekiri kufanya mashambulizi hayo  katika ngome za Hezbollah ikiwemo maghala ya silaha mjini Beirut.