Janabi ahadharisha vifo magonjwa yasiyoambukiza

MKURUGENZI Mtendaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Profesa Mohamed Janabi amehimiza jamii kubadili mtindo wa maisha kuepuka vifo vinavyosababishwa na magonjwa yasiyoambukiza.

Profesa Janabi alisema hayo katika kipindi cha Busati la Mtoro kilichorushwa na kituo cha televisheni cha ZBC2 jana jioni.

Alisema ugonjwa wa moyo unaua watu milioni 18 duniani kila mwaka na shinikizo la damu la juu linaua watu milioni 9.4 kila mwaka duniani.

Profesa Janabi alisema ugonjwa wa shinikizo la damu umekuwa tishio nchini kwa sababu kila wanaume wanne mmoja wao ana shinikizo la juu la damu bila kujijua hali ambayo ni ya hatari.

Ameonya matumizi ya chumvi nyingi akisema kila mtu anatakiwa kula chakula chenye chumvi ambayo hawezi kuihisi mdomoni. Alisema kuwa chumvi ni kichocheo cha vifo vitokanavyo na shinikizo la juu la damu.

“Kuna watu wenye shinikizo la damu la juu lakini wao wenyewe hawajui kwa sababu hawana desturi ya kupima shinikizo la damu. Wapo wanaojua kuwa wana tatizo hilo lakini katika matumizi ya dawa hawatumii ipasavyo, mara leo katumia lakini kesho kaacha hali ambayo ni hatari sana,” alisema Profesa Janabi.

Aliongeza: “Ushauri wangu kwa wananchi, kila mwaka wajenge utaratibu wa kupima shinikizo la juu la damu ili kuokoa afya kwani taratibu linaua macho, linaua nguvu za kiume”.

Profesa Janabi alisema hakuna dalili mahususi inayoashiria kuwa na shinikizo la damu, hivyo wananchi wanatakiwa kutoishi kwa mazoea kuwa akihisi vinginevyo anajua ni shinikizo la damu.

Alisema ugonjwa wa kiharusi unaua watu milioni 6.5 kila mwaka duniani.

Profesa Janabi alisema kiharusi kinasababishwa na shinikizo la juu la damu na vipo vya aina mbili.

Kipo kiharusi kinachosababishwa na kupasuka kwa mshipa kichwani ambacho ndicho kibaya zaidi na aina ya pili ni kiharusi kinachosababishwa na kuminywa kwa mshipa unaopeleka damu kichwani.

Kuhusu ugonjwa wa saratani, alisema unaua watu milioni 9.6 kila mwaka duniani.

“Ugonjwa mwingine ni wa figo ambao umeathiri watu zaidi ya milioni 850 duniani. Ugonjwa mwingine ambao umekuja karibuni ni mpya ni afya ya akili ambao unaua watu milioni moja kila mwaka duniani,” alisema Profesa Janabi.

Pia, alisema watu zaidi ya milioni 2.5 wanafariki dunia kila mwaka kutokana na matatizo ya njia ya chakula kutoka mdomoni hadi kwenye haja kubwa.

Profesa Janabi alisema ajali za barabarani limekuwa tatizo lingine kwa kuwa kila mwaka watu milioni 1.3 wanapoteza maisha na zaidi ya milioni 50 wanapata ulemavu.

Alisema uvutaji wa sigara unaangamiza watu zaidi ya milioni saba duniani kila mwaka kutokana na kusababisha saratani na pumu. Aidha, watu milioni 1.2 wanaokaa karibu na wavuta sigara wanakufa kila mwaka.

Kwa upande wa kisukari, Profesa Janabi alisema ugonjwa huo upo wa aina mbili kwa maana ya aina ya kwanza ya kuzaliwa na aina ya pili inayosababishwa na mtindo wa maisha.

Habari Zifananazo

3 Comments

  1. Инженерное оборудование для водоподготовки играет важную роль в обеспечении людей и производственных предприятий качественной питьевой
    водой. Водоподготовка включает несколько шагов, таких как пропускание через фильтры, умягчение, обеззараживание и удаление
    недопустимых примесей. Для этих целей применяются разнообразные устройства и системы, которые позволяют надежно очищать воду, делая её
    пригодной для обслуживания.

    Одним из важных элементов водоподготовки являются очистительные устройства, которые
    могут быть физическими, угольными, железообезжелезными
    и все прочие. Механические фильтры используются для удаления
    твердых частиц, таких как песок и грязь, в то время как
    угольные фильтры обеспечивают удаление природных загрязнителей и хлора.
    Железообезжелезные установки
    необходимы для удаления повышенного железа и марганца, что особенно актуально в районах
    с высоким содержанием этих элементов в воде.

    Кроме того, для доработки качества воды
    применяются системы умягчения, которые устраняют твердость воды, вызванную присутствием кальция и магния.

    Умягчение воды может быть достигнуто с помощью химических смол, которые заменяют эти элементы на натрий.
    Такое оборудование помогает увековечить
    срок службы приборов, а также уменьшить образование накипи.

    Современные технологии пастеризации, такие как ультрафиолетовое излучение
    и озонирование, активно используются для уничтожения микробов
    и патогенных микроорганизмов в
    воде. Эти методы являются экологичными для человека и не оставляют негативных побочных продуктов, что делает их предпочтительными для обеспечения высокого
    качества питьевой воды в любых
    условиях.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button