Jela miaka 60 kwa kumpa mimba mwanafunzi

RUVUMA; Tunduru. MAHAKAMA ya Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma, imemhukumu  kifungo cha miaka 60 Jela,  Faraji Milanzi  Yasini (20), mkulima na mkazi  wa Kijiji cha Ruanda – Mkowela, wilayani Tunduru, baada ya kupatikana na hatia ya kubaka  na kumpa mimba mwanafunzi.

Akisoma hukumu hiyo kesi namba 62  ya mwaka 2023, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Honorius Kando alisema Mahakama imefikia uamuzi huo baada ya kujiridhisha na ushahidi uliotolewa pasipo shaka yoyote na kumtia hatiani mtuhumiwa huyo.

Mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo Novemba  10, 2022 Kijiji cha  Ruanda -Mkowela ambapo amehukumiwa miaka 30 kwa kila kosa.

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button