Kitayosce, Fountain Gate zafungiwa usajili

KLABU ya Kitayosce inayoshiriki ligi kuu Tanzania bara pamoja na Fountain Gate inayoshiriki ligi ya Championship zimefungiwa kusajili wachezaji kutokana na kushindwa kumlipa aliyekuwa Kocha wao.

Taaarifa iliyotolewa na shirikisho la soka Tanzania TFF leo Julai 12 imesema uamuzi huo umekuja baada ya kocha Ahmed El Faramawy Yousef kushinda kesi ya madai dhidi ya klabu hizo.

Kocha huyo raia wa Misri ambaye alizifundisha timu hizo kwa vipindi tofauti alifungua kesi FIFA akipinga kuvunjiwa mkataba kinyume cha taratibu.

Taaarifa hiyo ya TFF imesema baada ya kocha huyo kushinda kesi yake timu hizo zilipaswa kumlipa ndani ya siku 45 lakini zimeshindwa kufanya hivyo na shirikisho la soka ulimwenguni FIFA limezifungia kufanya usajili wa kimataifa huku TFF ikizifungia kufanya usajili wa ndani.

Aidha TFF wamezitaka timu mbalimbali kuzingatia vipengele vya kimkataba kabla ya kuvunja mkataba na makocha au wachezaji.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Patricia J. Sawyers
Patricia J. Sawyers
2 months ago

online job from home. Last month i have earned and received $16650 from this job-home- by giving this only 3 hrs a a day.Every person can now get this job and start earning online by follow details.
🙂 GOOD LUCK.:)
.
.
.
HERE——➤ https://fastinccome.blogspot.com/

LaraKerr
LaraKerr
2 months ago

I make 100 bucks per hours while I’m courageous to the most distant corners of the planet. Last week I worked on my PC in Rome, Monti Carlo at the long final in Paris. This week I’m back inside the USA. All I do fundamental errands from this one cool area see it. For more information,

Click on the link below………… https://Bestdollar4.blogspot.Bom

Last edited 2 months ago by LaraKerr
Back to top button
2
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x