Lebron aweka rekodi NBA

Lebron James ameingia kwenye rekodi ya kuwa mfungaji bora wa NBA kwa kuwa na pointi 38, 390 akimpita Kareem Abdul-Jabbar mwenye poinit 38,387.

Nyota huyo wa Lakers amefikisha pointi hizo usiku wa kuamkia leo wakati timu yake ilipofungwa na Oklahoma City Thunder 133-130 katika pointi hizo Lebron alifunga 38.

Lebron alifunga pointi 20 katika kipindi cha kwanza na akavunja rekodi katika robo ya tatu ya pointi 16 zikiwa zimesalia sekunde 10.9 kuisha. robo ya tatu alifikisha jumla ya pointi 38,388 na kuvunja rekodi ambayo Kareem Abdul-Jabbar alishikilia kwa takriban miongo minne.

Advertisement

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 38 alikuwa akiuguza kifundo cha mguu wakati wa maandalizi ya mchezo.

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *