Mafunzo kupunguza madhara ya kisaikolojia waathirika ukatili

DODOMA: Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto kwa kushirikiana na Irish Rule of Law International, kwa ufadhili wa Ubalozi wa Ireland nchini Tanzania, vinaendesha mafunzo ya siku tatu kwa mahakimu na maofisa ustawi wa jamii kuhusu mbinu za kuepuka kuwasababisha waathirika wa ukatili wa kingono majeraha ya kisaikolojia wakati wa mchakato wa utoaji haki.
Mafunzo hayo yamezinduliwa jijini Dodoma na yanalenga kuwajengea washiriki ujuzi wa kutumia lugha ya staha, kuendesha mashauri kwa weledi, na kuandaa mazingira salama ya kimahakama kabla, wakati na baada ya ushahidi. Pia yameelezwa kuwa muhimu katika kupunguza hofu na maumivu ya ziada kwa manusura wanaposhiriki kwenye kesi za ukatili wa kingono.

Akifungua mafunzo hayo, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania kanda husika alisisitiza umuhimu wa mifumo rafiki ya utoaji haki kutokana na athari kubwa za kihisia na kisaikolojia zinazosababishwa na ukatili wa kijinsia. Kwa upande mwingine, katika Kituo Jumuishi cha Masuala ya Mirathi na Familia – Temeke, msisitizo uliwekwa kwenye umuhimu wa kulinda utu wa manusura katika hatua zote za kesi.
Mahakama Kuu ya Tanzania kupitia watendaji wake pia imeendelea kuhimiza matumizi ya mbinu zisizo za kuumiza zaidi (trauma-informed approaches) katika mfumo wa haki.

Mafunzo haya ya awamu ya sita yanawakutanisha washiriki 60 kutoka mikoa mbalimbali, ambapo kundi la Dodoma linahusisha washiriki kutoka Iringa, Tabora, Manyara, Arusha, Moshi na Dodoma, huku kundi la Dar es Salaam likihusisha washiriki kutoka Pwani, Tanga, Lindi, Songea, Mtwara na Morogoro.
Dar es Salaam pia ni moja ya vituo vya utekelezaji wa mafunzo haya, kupitia kundi la pili la washiriki.




Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily…………
.
More Details For Us→→→→ https://Www.Payathome9.Com
It’s amazing to pay a visit this web page and reading the views of all mates concerning this post, while I am also keen of getting experience.