Marekani yadhibiti sheria za TikTok

WASHINGTON DC : SERIKALI ya Marekani imetangaza kuwa makampuni ya Marekani yatadhibiti mchakato wa kanuni za kompyuta (algorithm) za TikTok nchini humo kupitia mkataba mpya unaotarajiwa kusainiwa na China.

Waziri wa Vyombo vya Habari, Karoline Leavitt, amesema makubaliano hayo yanaweza kusainiwa katika siku zijazo ingawa Beijing bado haijatoa tamko rasmi. SOMA: TikTok yapata mnunuzi, majina yahifadhiwa

Marekani imekuwa ikishinikiza kampuni mama ya TikTok, ByteDance, kuondoa ushiriki wake katika shughuli za programu hiyo nchini Marekani kwa sababu za usalama wa taifa. Hapo awali, TikTok iliagizwa kuuza shughuli zake au kukabili hatari ya kufungiwa.

Hata hivyo, Rais Donald Trump amechelewesha mara nne kutekeleza marufuku hiyo tangu Januari na wiki hii ameongeza muda hadi Desemba. Leavitt alisema usimamizi wa data na faragha za watumiaji wa Marekani utaongozwa na kampuni kubwa ya teknolojia, Oracle, inayoongozwa na bilionea Larry Ellison.

 

Habari Zifananazo

2 Comments

  1. I honestly didn’t expect much when I first tried this, but here I am making around 6,854/USD a month just by working online a few hours a day from home. It’s not a get-rich scheme, just something steady that’s been working for me quietly in the background. If you’ve been looking for something consistent like I was, here’s what I started with:
    👉 https://www.jobs67.com

  2. Google pays $300 on a regular basis. My latest salary check was $8600 for working 10 hours a week on the internet. My younger sibling has been averaging $19k for the last few months, and he constantly works approximately 24 hours. I’m not sure how simple it was once I checked it out.

    This is my main concern………………. http://Www.Cash43.Com

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button