Mbunge Bukoba Mjini awafikia wenye uhitaji

BUKOBA: Mbunge wa Jimbo la Bukoba Mjini, Johnston Mutasingwa, ametoa msaada kwa makundi maalumu pamoja na wanufaika wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) Kata ya Kibeta katika kipindi mwezi wa Ramadhan na Kwaresma.
Mahitaji yaliyotolewa ni sukari, sabuni na vyakula mbalimbali vya kusaidia familia kipindi cha mfungo. Msaada huo ulikabidhiwa na katibu wake Hamada Simba.

Simba amesema msaada huo unalenga kuwasaidia wananchi walio katika mazingira magumu, wakiwemo wazee, watu wenye ulemavu pamoja na kaya zenye kipato cha chini zinazofaidika na mpango wa TASAF.

Wananchi walionufaika na msaada huo walionyesha furaha na shukrani zao za dhati kwa mbunge wao, wakisema kuwa hatua hiyo imewapa faraja kubwa na kuwasaidia kukabiliana na changamoto za maisha ya kila siku.
“Tunamshukuru sana mheshimiwa mbunge kwa kutujali, msaada huu umekuja wakati sahihi na utatusaidia sana katika maisha yetu,” amesema mmoja wa wanufaika.

Diwani wa Kata kibeta, Anastella Alphuns amesema kuwa kwa ujumla, tukio hilo limeendelea kuonesha mshikamano kati ya viongozi na wananchi pamoja na juhudi zinazoendelea za kuhakikisha ustawi wa jamii unaimarika, hasa kwa makundi yenye uhitaji zaidi.





JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 12000-16700 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..
.
This is my main concern…………………… http://Www.Cash54.Com
I just came across this amazing way to earn $11,000-$15,000 a month online! No selling, no struggle—just a simple system that anyone can follow. Mia Westbrook did it, and so can you! Don’t miss out on this life-changing opportunity.
.
This is what I do…………………… http://Www.Payathome9.Com