MOI yaanza upasuaji kurekebisha viungo

KWA mara ya kwanza, Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) imeanza kutoa huduma za upasuaji wa kibingwa wa kutibu mishipa ya fahamu iliyoathirika kutokana na ajali katika mikono na miguu kwa wagonjwa wanaokabiliwa na changamoto hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa MOI, Balozi Dk. Mpoki Ulisubisya amesema hatua hiyo ni mafanikio makubwa kwa taasisi hiyo na sekta ya afya nchini kwa ujumla. “Tumeanza kwa mafanikio kutibu mishipa ya fahamu iliyopo mikononi na miguuni. Huduma hii itawanufaisha wagonjwa wanaoshindwa kuinua vitu au wanaopata changamoto ya kutembea vizuri baada ya kupata ajali,” amesema Dk. Mpoki.

Ameongeza kuwa kwa sasa huduma hiyo inapatikana MOI pekee nchini, baada ya madaktari wa taasisi hiyo kupata mafunzo ya ubobezi na ujuzi maalum wa kufanya upasuaji huo. “Huduma hii imeanza baada ya daktari wetu kukamilisha masomo ya ubobezi na kupata utaalamu wa kutibu na kufanya upasuaji wa mishipa ya fahamu iliyopata majeraha,” ameongeza.

Kwa upande wake, Daktari Bingwa Bobezi wa Majeraha ya Mkono na Mguu, Dk. Hellen Machagge, amesema kuwa kujeruhiwa kwa mishipa mikubwa ya fahamu husababisha misuli midogo kushindwa kufanya kazi, hali inayoweza kusababisha kupooza kwa mikono au miguu.

“Katika upasuaji huu tunahamisha mishipa ya fahamu kutoka sehemu moja kwenda sehemu iliyoathirika ili kuuwezesha mkono au mguu kuanza kufanya kazi vizuri kama ilivyokuwa kabla ya kujeruhiwa,” amesema Dk. Hellen.

Hatua hiyo ni muendelezo wa MOI kuanzisha huduma za kibingwa na kibobezi ambazo hazikuwapo nchini, na hivyo kupunguza usumbufu pamoja na gharama kubwa za wagonjwa waliolazimika kufuata huduma hizo nje ya nchi. SOMA: MOI yagawa viungo bandia bure

Habari Zifananazo

2 Comments

  1. I just came across this amazing way to earn $6,000-$8,000 a week online! No selling, no struggle—just a simple system that anyone can follow. Mia Westbrook did it, and so can you! Don’t miss out on this life-changing opportunity.
    .
    Follow Here ……………………… https://Www.Cash54.Com

  2. I get paid over 220 Dollars per hour working from home with 2 kids at home. i never thought i’d be able to do it but my best friend earns over 15k a month doing this and she convinced me to try. it was all true and has totally changed my life. This is what I do, check it out by Visiting Following Website…

    .
    M­­­­­­o­­­­­­r­­­­­­e­ D­­­­­­e­­­­­­t­­­­­­a­­­­­­i­­­­­­l­­­­­­s For Us→→→→→→→→→ https://Www.Payathome9.Com

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button