NEMC yashiriki mkutano wa UNOC3 Ufaransa

BARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashiriki mkutano wa Tatu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Usimamizi wa Bahari (UNOC3) unaofanyika jijini Nice, Ufaransa kuanzia Juni 9 hadi 13, 2025.

Mkutano huo unaohudhuriwa na Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dk Immaculate Sware Semesi ambapo kwa Tanzania umewakilishwa na Makamu wa Rais Dk Philip Isdor Mpango umelenga kujadili na kuhamasisha utekelezaji wa mpango mkakati wa maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UN-SDG-14).

Kwa mwaka 2025 Mkutano huo umebeba Kaulimbiu, “๐‚๐ก๐จ๐œ๐ก๐ž๐š ๐ก๐š๐ญ๐ฎ๐š ๐ณ๐š ๐ก๐š๐ซ๐š๐ค๐š ๐ง๐š ๐ฎ๐ฌ๐ก๐ข๐ซ๐ข๐ค๐ข๐š๐ง๐จ ๐ฐ๐š ๐ฐ๐š๐๐š๐ฎ ๐ฐ๐จ๐ญ๐ž ๐ค๐š๐ญ๐ข๐ค๐š ๐ค๐ฎ๐ก๐ข๐Ÿ๐š๐๐ก๐ข ๐ง๐š ๐ฆ๐š๐ญ๐ฎ๐ฆ๐ข๐ณ๐ข ๐ž๐ง๐๐ž๐ฅ๐ž๐ฏ๐ฎ ๐ฒ๐š ๐๐š๐ก๐š๐ซ๐ข” ambayo inalenga kuhamasisha wahusika wote kuhifadhi na kutumia Bahari kwa maendeleo endelevu.

Mkutano huo pia umewakutanisha viongozi wakuu wa nchi na Serikali wa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa, Mashirika ya Kimataifa, Taasisi, Asasi za kiraia pamoja na Sekta binafsi.

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button