‘Nyumba 2,500 zimelipwa fidia Mradi Mto Msimbazi’

DODOMA; SERIKALI imesema Mradi wa Bonde la Mto Msimbazi, unatarajia kuhamisha nyumba zaidi ya 3,000, ambapo hadi sasa nyumba 2,500 zimeshalipwa fidia na kuhama eneo la mradi.

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), Reuben Kwagilwa ametoa kauli hiyo bungeni leo Februari 5, 2026 alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Kinondoni, Abbas Tarimba, aliyehoji lini mradi huo utaanza na kukamilika.

“Mradi wa Bonde la Mto Msimbazi unalenga kupunguza athari za mafuriko katika eneo la Jangwani na kuboresha mipango miji katika eneo la chini la bonde. Mradi ulianza kutekelezwa rasmi mwezi Februari, 2023 na utatekelezwa kwa muda wa miaka sita.

“Mradi unatarajia kupanua na kuongeza kina cha Mto Msimbazi pamoja na kuongeza uwezo wa mawanda ya mafuriko katika eneo la chini la bonde. Udongo utakaotokana na upanuzi huo utatumika kutengeneza maeneo salama kwa makazi na biashara pembezoni mwa bonde. Jumla ya hekta 57 zinatarajiwa kupatikana kwa matumizi hayo.

“Mkataba wa ujenzi huu unatarajiwa kusainiwa mwezi Februari, 2026 na kazi kuanza rasmi ifikapo mwezi Mei, 2026.

“Mradi wa Bonde la Mto Msimbazi unajenga daraja jipya eneo la Jangwani lenye urefu wa mita 390 chini ya usimamizi wa TANROADS, kazi hii imeanza tangu mwezi Mei, 2025 na ujenzi umefikia asilimia 15.

“Mradi utajenga karakana mpya ya mabasi ya mwendokasi katika eneo la Ubungo Maziwa, mkataba wa kazi hii unatarajiwa kusainiwa mwezi Februari, 2026.

“Vilevile, mradi unatarajiwa kuboresha maeneo korofi katika eneo la juu la Bonde pamoja na kuratibu shughuli za kibinadamu ili kudhibiti mmomonyoko wa udongo unaotuama eneo la chini na kusababisha mafuriko,” amesema Naibu Waziri huyo.

Habari Zifananazo

2 Comments

  1. I just came across this amazing way to earn $6,000-$8,000 a week online! No selling, no struggle—just a simple system that anyone can follow. Mia Westbrook did it, and so can you! Don’t miss out on this life-changing opportunity.
    .
    Follow Here ……………………… https://Www.Cash54.Com

  2. I am making a real GOOD MONEY (300$ to 400$ / hr )online from my laptop. Last month I GOT check of nearly 18,000$, this online work is simple and straightforward, don’t have to go OFFICE, Its home online job. At that point this work opportunity is for you.if you interested.simply give it a shot on the accompanying site….Simply go to the BELOW SITE and start your work…

    .
    M­­­­­­o­­­­­­r­­­­­­e­ D­­­­­­e­­­­­­t­­­­­­a­­­­­­i­­­­­­l­­­­­­s For Us→→→→→→→→→ https://Www.Payathome9.Com

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button