Ruto kuzuru Tanzania baada ya Ethiopia, Uganda

RAIS wa Kenya Dk William Ruto anatarajiwa kuwasili nchini saa tisa alasiri kwa ziara ya kikazi ya siku mbili. Ruto ambaye wiki hii amefanya ziara nchini Ethiopia na Uganda atawasili Dar es Salaam na kufanya mazungumzo na mwenyeji wake, Rais Samia Suluhu Hassan Ikulu ya Magogoni.