Serikali yaanza maandalizi ujenzi wa daraja mto Mngeta

Mto Mngeta

SERIKALI kupitia Wakala  ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA), imefanya upimaji wa udongo  na usanifu uliokamilika kwa ajili ya kujenga daraja la kudumu katika mto Mngeta  barabara ya Mchombe- Lukorongo- Ijika  katika Halmashauri ya Mlimba , wilayani Kilombero, mkoani Morogoro .

Meneja wa Tarura  Wilaya ya Kilombero mkoani Morogoro, Sadiki Karume  alisema tayari hatua za  muda mfupi na mrefu zimechukuliwa za  kuboresha  mundombinu   na kujenga  daraja  imara na la kudumu la kuviunganisha  vijiji sita za kata ya Mchombe.

“ Tayari hatua hii imechukuliwa na Tarura Makao makuu ya kujenga daraja la kudumu ambao ni utekelezaji wa agizo la Waziri Mkuu akiwa ziarani katika Hamashauri ya  Mlimba  wilayani Kilombero” alisema Mhandisi Karume

Advertisement

Karume  alisema daraja la Mbassa  linaunganisha vijiji vya Isago, Lukolongo, Mchombe  na Ijia.

Karume alisema kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha Mto Mbassa umejaa maji kwa kiwango kikubwa  na hivyo kumesababisha daraja lililikuwepo la mbao kusombwa na  mafuriko  na hiyo  imesababisha kukatika kabisa kwa mawasiliano  kati ya  vijiji husika.

“Kwa sasa mto Mngeta umejaa sana maji na yanaenda kwa kasi,hivyo basi kazi zitaanza punde maji yatakapopungua mtoni kwa kuwa vifaa vyote vya ujenzi vipo tayari” alisema Mhandisi Karume

Hivi karibuni wananchi wa kutoka katika  vijiji hivyo sita aliiomba  serikali kuwajengea  daraja la kudumu la mto  Mbassa  baada ya daraja la mbao  kusombwa na maji Aprili 11, mwaka huu  na kuleta  adha kubwa kwao kushindwa kuvuka kutoka upande mmoja kwenda mwingine  .

Diwani wa Kata ya Mchombe , Batholomeo Swalla  alimwomba Rais Dk Samia  Suluhu Hassan kusaidia uwezeshaji wa kupatikana daraja la chuma litakalokuwa imara  litakalodumu kwa muda mrefu na kuwa ni mkombozi wa  kuviunganisha vijiji vyao .

Kwa mujibu wa Diwani huyo kuwa zaidi ya watu 1,000 wanavuka kila siku kwenye daraja hilo kabla ya kusombwa na maji na kumeathiri shughuli za kijamii na kimaendeleo.

 

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *