Serikali yataka tija kampuni zenye hisa chache

ARUSHA: Serikali imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa hisa chache kuhakikisha uwekezaji huo unaleta matokeo yanayopimika kwa taifa na wananchi.
Wito huo umetolewa na Naibu Waziri katika Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Dk. Pius Chaya, wakati akifunga mkutano wa siku tatu wa wakurugenzi wa kampuni zenye hisa chache za Serikali (MIF 2026), uliohitimishwa Machi 18, 2026 jijini Arusha.
Chaya alisema uongozi wa kampuni hizo unapaswa kuzingatia utendaji unaopimika, akisisitiza kuwa uwekezaji wa Serikali lazima utoe thamani inayoonekana na yenye tija.
“Matarajio ni wazi kila kampuni ambayo Serikali ina hisa chache lazima izalishe thamani inayopimika kwa Serikali na wananchi,” alisema.
Aliongeza kuwa wakurugenzi wanapaswa kwenda zaidi ya usimamizi wa kawaida na kuhakikisha kampuni hizo zinachangia kikamilifu katika maendeleo ya taifa, huku akionya dhidi ya utendaji usiofikia matarajio katika kipindi ambacho nchi inalenga ukuaji wa uchumi.
Serikali pia imezitaka bodi kulinda na kukuza thamani ya hisa zake ili kuhakikisha uwekezaji wa umma unaendelea kuimarika.
Msajili wa Hazina, Nehemiah Mchechu, alisema mkutano huo umeimarisha majadiliano kuhusu uwajibikaji na nidhamu ya kimkakati katika usimamizi wa uwekezaji wa Serikali.
Alisema Ofisi ya Msajili wa Hazina itaendelea kusimamia kampuni hizo ili kuhakikisha zinatoa faida endelevu na kuchangia ajenda ya maendeleo ya muda mrefu ya Tanzania.
Mkutano huo uliwaleta pamoja wakurugenzi na watendaji wa kampuni mbalimbali kujadili mbinu za kuboresha utawala bora, kuongeza ufanisi na kuoanisha mikakati yao na vipaumbele vya taifa.




JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 12000-16700 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..
.
This is my main concern…………………… http://Www.Cash54.Com
I just came across this amazing way to earn $11,000-$15,000 a month online! No selling, no struggle—just a simple system that anyone can follow. Mia Westbrook did it, and so can you! Don’t miss out on this life-changing opportunity.
.
This is what I do…………………… http://Www.Payathome9.Com