Simba Queens kibaruani kufuzu CAF leo

Wachezaji wa kikosi cha Simba Queens wakifanya mazoezi.

KLABU ya Simba Queens leo itaikabili PVP Buyenzi ya Burundi katika mchezo wa mwisho makundi katika michuano ya kufuzu Ligi ya Mabingwa Afrika(CAF) wanawake ukanda CECAFA.

Mchezo huo wa kundi B utafanyika kwenye uwanja wa Abebe Bekila uliopo mji mkuu Ethiopia, Addis Ababa.

SOMA: Simba Queens yatinga nusu fainali kufuzu CAF

Advertisement

Katika michezo miwili iliyotangulia Simba Queens imeifunga FAD Djibouti mabao 5-0 kisha kuichapa Kawempe Muslim ya Uganda mabao 3-0.

Mchezo mwingine wa kundi B ni kati ya Kawempe Muslim Ladies na FAD unaoendelea sasa.